Breaking News

Your Ad Spot

Mar 24, 2014

BODI YANG'OA MKURUGENZI TTB

Na Mwandishi wetu
BODI ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imemshauri Waziri wa Maliasili  na Utalii, Lazaro Nyalandu kumuondoa kazini Murugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Dk. Aloyce Nzuki kutokana na utendaji usioridhisha.


Katika kikao cha pamoja kati ya bodi hiyo na Nyalandu pamoja na Naibu  wake Mahamoud Mgimwa, Katibu Mkuu Maimuna Tarishi na Naibu Katibu Mkuu, Selestine Gesimba, waziri aliridhia uamuzi wa bodi, ambapo alisema Dk. Nzuki atapangiwa kazi nyingine.


Mwenyekiti wa Bodi hiyo Charles Sanga, ndiye alitangaza uamuzi huo akisema ni vema Dk. Nzuki akaondolewa kwa sababu hawataweza kufanya naye kazi.


Alisema utaifa na uzalendo ni kiti kizuri kwa watanzania na pia bodi yao inafanya kazi kwa ufanisi kwa ajili ya wananchi na madaraka ni dhamana, hivyo hawataweza kufanya kazi na Dk. Nzuki.


Nyalandu alisema aliridhia uamuzi huo baada ya kupokea barua kutoka Bodi ambayo ilisainiwa na wajumbe hao ikimshauri amuondoe Dk. Nzuki kutokana na kutokuwa na imani naye.


Baada ya kuridhia uamuzi huo aliiagiza bodi kuitangaza nafasi hiyo kwa watanzania wenye sifa duniani kote na waombe kazi hiyo ndani ya siku 21 kuanzia leo.


Aidha, Nyalandu alisema nafasi hiyo kwa sasa itakaimiwa na Mkurugenzi wa Masoko, Devota Mdachi hadi hapo mchakato wa kumpata mkurugenzi utakapokamilika.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages