Breaking News

Your Ad Spot

Mar 25, 2014

VIONGOZI WA KAMATI 12 ZA BUNGE MAALUM LA KATIBA NA KAMATI YA UONGOZI YATAJWA

DODOMA, Tanzania
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Mhe. Samwel Sitta leo, ametangaza majina ya wenyeviti na makamu wenyeviti wa Kamati za bunge hilo.

Majina hayo yametangazwa na Mwenyekiti huyo  baada ya uchaguzi wa viiongozi hao uliofanyika  (jana) Machi 24 , mwaka  2014 mjini  Dodoma .

Mwenyekiti huyo aliyataja majina hayo  katika  Kamati  ya Uandishi Mwenyekiti    Andrew Chenge, Makamu wake ni Mgeni Hassan Juma. Kamati ya Kanuni Mwenyekiti ni Pandu Ameri Kificho, Makamu wake ni Dkt. Susan Kolimba. Kamati Na. 1 Mwenyekiti ni  Ummy Ally Mwalimu, na Makamu wake ni  Prof. Makame  Mbalawa.

Wengine waliochaguliwa  katika Kamati Na. 2 Mwenyekiti ni Shamsi Vuai Nahodha, Makamu wake ni  Shamsa Mwangunga.Kamati Na. 3 Mwenyekiti         ni  Dkt. Francis Michael, Makamu wake ni Fatma MussaJuma.
Mhe. Sitta alisema waliochaguliwa katika Kamati Na. 4 Mwenyekiti ni  Christopher  Ole-Sendeka, Makamu wake ni  Dkt. Sira Ubwa Mamboya, Kamati Na. 5 Mwenyekiti ni  Hamad Rashid Mohamed Makamu wake ni  Assumpter  Mshama.

          Viongozi waliochaguliwa katika Kamati Na. 6 Mwenyekiti Stephen Wassira na Makamu wake ni Dkt. Maua                   Daftari.Kamati Na. 7  Mwenyekiti  Brig. Hassan Ngwilizi  ,Makamu wake  Waride                                    BakariJabu.Kamati Na. 8 Mwenyekiti           ni Job Ndugai,Makamu wake ni Biubwa Yahya   Othman.
Kamati Na. 9 Mwenyekiti ni Kidawa Hamidi Saleh,Makamu wake Wiliam  Ngeleja,Kamati Na. 10 Mwenyekiti ni Anna  Abdallah, Makamu wake ni   Salmin Awadh Salmin.Kamati Na. 11 Mwenyekiti ni  Anne  Malecela, Makamu wake  Hamad  Masauni na Kamati Na. 12 Mwenyekiti                           Paul  Kimiti na Makamu wake ni  Thuwaybah E. Kisasi.

Wakati huohuo , Sitta  alitangaza wajumbe wa Kamati ya  Uongozi ya Bunge Maalum la Katiba, ambao  ni wenyekiti na makamu wenyeviti wa kamati hizo wakiwemo wajumbe wengine watano aliowateua.
 Wajumbe hao walioteuliwa na Sitta kuingia katika kamati hiyo ni Fakharia Khamisi Shomari, Mary Chatanda, Profesa Ibrahim Lipumba, Amon Mpanju na Hamad Abuu Juma.

 Hata hivyo pamoja na majina hayo kutangazwa Profesa Lipumba alisimama na katika nafasi hiyo .

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages