Breaking News

Your Ad Spot

Apr 28, 2014

BENKI YA POSTA TANZANIA YATOA MSAADA VITU MBALIMBALI KWA WODI YA WATOTO WENYE MAGONJWA YA SARATANI MUHIMBILI


 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Mystica Ngongi akimkabidhi hundi ya sh. milioni 2 Mkuu wa Idara ya Ustawi ya Jamii Hospitali ya Taifa Muhimbili, Beatrice Mugula kwa ajili ya wagonjwa wa saratani watoto waliolazwa katika hospitali hiyo. Kushoto ni Meneja Mahusiano Mwandamizi TPB, Noves Moses. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Mystica Ngongi (wa pili kushoto) akimkabidhi sehemu ya msaada wa nguo, madaftari, sabuni, vitabu vya watoto, Meneja wa jengo la watoto katika hospitali ya Muhimbili, Praxeda Chenya kwa ajili ya kusoma vikiwa na thamani ya sh. milioni moja, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sikukuu ya Muungano. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Mahusiano Mwandamizi TPB, Noves Moses na wa pili kulia ni Mkuu wa Idara ya Ustawi ya Jamii Hospitali ya Taifa Muhimbili, Beatrice Mugula. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
 
Wafanyakazi wa TPB wakiweka sawa zwadi kabla ya kuzikabidhi.

 Wafanyakazi wa Benki ya Posta na watoto waliolazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili katika picha ya Pamoja.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages