Breaking News

Your Ad Spot

Apr 16, 2014

KINANA AZINDUA MRADI WAUJENZI NYUMBA 60 INYONGA KATIKA WILAYA MPYA YA MLELE UNAOFANYWA NA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 60 za makazi ya watu zinazojengwa na Shirika la Nyumba ya Taifa katika Wilaya ya Mlele mkoani Katavi.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana  akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Shirika la Nyumba Mkoa wa Katavi, Nehemia Msigwa juu ya miradi ya ujenzi wa nyumba itakayofanyika ndani ya mkoa wa Katavi.
 Michoro ya nyumba zitakazojengwa mkoani Katavi na Shirika la Nyumba ya Taifa,ambapo wilaya ya Mlele ,Shirika la Nyumba linajenga nyumba 60 na zitachukua  miezi nane kukamilika.
 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr. Rajab Rutengwe  akizungumza mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la uzinduzi wa nyumba 60 zitakazojengwa na Shirika la Nyumba  la Taifa  katika wilaya ya Mlele.
Meneja wa Huduma za Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa Ndugu Muungano Saguya akizungumzia namna Shirika la Nyumba lilivyojipanga katika kuboresha makazi ya watu katika mkoa wa Katavi. Picha na Adam Mzee

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages