Breaking News

Your Ad Spot

Apr 25, 2014

VIJANA WAFANYA MATEMBEZI YA UZALENDO DAR


 Vijana wakiwa kwenye matembezi ya Uzalendo yalioratibiwa na Umoja wa Vijana wa CCM kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Matembezi hayo ambayo yalianzia Ofisi ya CCM Wilaya ya Temeke  hadi kwenye viwanja vya Maonyesho ya Mwalimu Nyerere vya sabasaba yalipokewa  na Rais Dk. Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein.
 Vijana wakionyesha ukakamavu huku wakidhihirisha Utanzania wao wakati wakiwa kwenye matembezi hayo
  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakishiriki matembezi hayo
 Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida wakati wakisubiri mapokezi ya matembezi hayo
 Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma Khamis akienda kukabidhi bendera ya Taifa kwa Rais Kikwete kwenye ukumbi wa PTA, mwishoni mwa matembezi hayo
Rais Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na picha ya  Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage huku Rais wa Zanzibar  Dk. Ali Mohamed Shein akiwa na picha ya  Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Abeid Amani Karume, baada ya vijana walioshiriki matembezi kuwakabidhi picha hizo.
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wananchi baada ya kupokea matembezi hayo ya Vijana katika Ukumbi wa PTA kwenye Viwanja vya Maonyesho ya sabasaba vya Mwalimu Nyerere
 Mamia ya watu wakimsikiliza Kikwete

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages