Breaking News

Your Ad Spot

May 26, 2014

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KUZURU SINGIDA VIJIJINI LEO

 Mbunge wa Singida Mashariki Lazaro Nyalandu akimlaki Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati wa mapokezi ya kiongozi huyo wa Chama,  katika kata ya Msisi, Singida Vijijini, leo Mei 26, 2014.
 Wanachama wa Jumuia ya Wazazi Kata ya Msisi wakimvalisha mgolole Kianana kabla ya kufungua tawi la Wazazi la Kata hiyo, leo, Mei 26, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizindua tawi la Jumuia ya Wazazi LKata ya Msisi, wilaya ya Singiga Vijijini, Mei 26, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akishiriki kuvuna mtama katika shamba la mfano la zao hilo katika kata ya Mtinko, Singida Vijijini, leo Mei 26, 2014. Aliyevaa suti ni Waziri wa maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Mashariki, Lazaro Nyalandu.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiwasha mashine ya kupukuchua mtama, wakati yeye na Kinana waliposhiriki uvunaji na upuchuaji mtama kwenye shamba darasa la zao hilo katika kata ya Mtinko, Singida Vijijini. leo Mei 20, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akishiriki kupukuchua mtama kwenye mashine maalum, katika Kata  hiyo, leo Mei 26, 2014.
 5Kinana na Nyalandu wakiweka dirisha kwenye jengo la mradi wa ushirika wa kusindika mafuta ya alizeti kata ya Mtinko
 Kinana akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Msisi katika mapokezi yake kuingia Singida Vijijini
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alimpatia chanjo ya matone, mtoto Erick Gabriel mwenye umri wa miezi miwili, aliyepatakwa na mama yake, Maria Jacob, Kiongozi huyo mkuu wa CCM, alipokagua huduma za  zahanati ya Mkenge, Singida Vijijini leo, Mei 26, 2014.
 Wananchi wakiwa nje ya Zahanati ya Mkange, Singida Vijijini, wakati Katibu Mkuu wa CCM, Kinana alipokagua zahanati hiyo mpya leo Mei 26, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiondoka na msafara wake  baada ya kukagua jengo la bweni la wanafunzi Maghojoa, Singida Vijijini leo Mei 26, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akiwa na Nyalandu wakati alipozungumza na wananchi baada ya kukagua ujenzi wa Ukumbi wa Ofisi ya CCM, Kata ya Maghojoa, Singida Vijijini.
 Nyalandu akisalimiana na wananchi wakati alipowasili na Kinana katika kata ya Mtinko, Singida Vijijini
Kinana akihutubia wananchi Kata ya Mtinko, Singida Vijijini. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages