Breaking News

Your Ad Spot

May 25, 2014

MASHINDANO YA DATS YAZINDULIWA MKOANI MOROGORO, MIKOA TISA KUSHIRIKI

 Mwenyekiti wa chama cha Dats Tanzania Gesase Waigama akiongea wakati wa ufunguzi wa mashindano ya mchazo huo unaoshirikisha mikoa  ya Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro, Kagera, Arusha na wenyeji wao Morogogoro ambapo katika mashindano hayo yaliodhaminiwa na bia aina ya Safari mshindi wa kwanza atatoka na kitita cha shilingi 600,000 hapo kesho.




 Baadhi ya washiriki wa mchezo huo wakifanya mazoezi kabla ya kuanza kwa shindano hilo linalofanyika katika ukumbi wa Magunila  Kihonda Mjini Morogoro.

 Wahsiriki wa shindano hilo kutoka mikoa mbailimbali wakiwa katika ukumbi  huo wakishuhudia pambano hilo.

 Irene Kihupi mchezaji kutoka mkoa wa Dar es Salaam akiwa katika pambano hilo.


 Joyce Laize mchezaji kutoka mkoa wa Arusha akiwa katika pambano hilo.


 Mwenyekiti huyo wa Dats akizindua mchezo huo ili kuruhusu pambano kuanza rasmi.


 Baadhi ya wachezaji wakiwa katika pambano hilo


Frolida Namajojo katibu wa Dats mkoa wa Morogoro akiwa katika mazoezi kabla ya kuanza mchezo huo.


WANACHAMA wa chama cha Darts Taifa (TADA) wameyaomba makampuni yanayodhamini michezo mbali mbli nchini kuwekeza kwenye chama hicho ili kuweza kukuza uchumi,michezo pamoja na kuongeza pato la taifa. 
Wanachama hao waliyasema hayo Mei 24 mwaka huu   kwa nyakati tofauti watika  wa mashindano ya mabingwa wa chama hicho yanayofanyika mkoani hapa.

Walisema kuwa mchezo huo ni mzuri lakini unachangamoto ya gharama ambapo alisema kuwa mara zote yanapoandaliwa mashindano hayo kila mwanachama anatakiwa kujitegemea mwenyewe. 
Aidha waliwaomba kopa Coca Cola kuandaa utaratibu wa kupeleka mchezo huo mashuleni ili kuweza kuibua vipaji vya mchezo huo kuanzia ngazi ya shule.

Kwa upande wake katibu mkuu wa chama hicho Kale Mwigonja alisema kuwa shindano hilo ambalo limedhaminiwa na kampuni ya bia ya Safari Lager linalenga kunua mchezo huoikiwa I pamoja na kujiandaa na Afrika Mashariki linalotarajia kufanyika mwezi juni mwaka huu Mkoani Dodoma. 
Alisema kuwa mashindano hayo yanashirikisha virabu 32 kutoka katika mikoa mbali mbali nchni ambapo alisema kuwa washindi watapata zawadi mbalimbali ikiwemo ikombe pamoja na zawadi za pesa taslimu ambapo alisema kuwa mshindi wa kwanza atapata sh.laki 6 na kikombe ,wa pili laki 4 na kikombe na watatu laki 3.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages