Rodney enzi za uhai wake.
MBUNIFU
na mwanamitindo (model) Rodrick Charles maarufu kwa jina la ‘Rodney de
lativo’ amefariki dunia jana (Mei 30) baada ya kuugua kwa muda alipokuwa
amelazwa Hospitali ya Jeshi, Lugalo.
Akizungumza
na Mtandao huu mapema leo kwa njia ya simu, Rafiki wa karibu wa
familia ya marehemu, David Msangi alisema marehemu alipatwa na umauti
alipokuwa akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Lugalo, alipokuwa
amelazwa na msiba huo hupo nyumbani kwa marehemu Tabata Bonyokwa, Dar.
“Tumempoteza
mtu muhimu sana ambaye alikuwa na mawazo mengi ya kufikia mafanikio
yake. Tutaendelea kumkumbuka.” Alisema Msangi ambaye pia alikuwa
mshahuri wa karibu wa marehemu", Msangi alisema.
Kwa mujibu wa familia ya marehemu, anatarajiwa kuzikwa hiyo Jumamosi Mei 31huko huko kwenye makaburi ya Tabata Segerea.
Wakati
wa uhai wake, marehemu alifanya kazi kwenye majukwaa mbalimbali na
wabunifu na wanamitindo wakubwa wakiwemo wabunifu Ally Remtullah,
Mustapha Hassanali, Asia Idarous. Wanamitindo Rio Poul, Martin Kadinda,
Justine, Faustine Simon na wengine wengi.
Rodney mpaka anakutwa na umauti, alikuwa mshahuri na model wa kampuni ya Crisswelly African Fashion. Mareehemu
alizaliwa Mei 26, 1994. Elimu yake alisomea Magoze Sekondari na
kuhitimu 2011 na kuingia moja kwa moja kwenye fani ya uwanamitindo na
kuendelea hadi alipokutwa na umauti.
Aidha,
kwa jamaa wa karibu na wabunifu na wanamitindo kwa watakaotaka maelezo
ya kufika kwa marehemu wanaweza kuwasiliana na David Msangi kwa namba
hii 0652901684
..Rest In Peace Rodney. I remember you forever.
Aidha kwa taarifa zaidi:
TAARIFA
ZA FAMILIA NI KWAMBA MSIBA UPO BONYOKWA JIJINI DAR ES SALAAM. PANDA
GARI YA TABATA SEGEREA SHUKA MWISHO WA GARI KISHA PANDA GARI ZA BONYOKWA
SHUKA MWISHO NDIPO MSIBA ULIPO WA NDUGU YETU MPENDWA RODNEY TUTA
MUHIFADHI KESHO SIKU YA JUMAMOSI SAA 9 ALASIRI UKIWA
NI MMOJA WAPO WA MDAU WA TANZANIA FASHION NA Crisswelly African
International Fashion, MODEL AU DESIGNER NIVEMA KUJITIKEZA NA KUSHIRIKI
KUMSINDIKIZA SAFARI YA MWISHO YA MPENDWA WETU RODNEY. PIA WAWEZA KUTUMA MCHANGO WAKO KWA MAMA Asya Khamsin KWA TIGOPESA NO0713263363
MUNGU AKUBARIKI TAFADHALI SHARE UJUMBE HUU KWA MARAFIKI ZAKO UTABARIKIWA AMEN!!!!!!!!!!!!!!
KWA MAELEZO WASILIANA NA #CRISSWELLY NO 0714802527
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269