Breaking News

Your Ad Spot

May 28, 2014

Serikali yafanikiwa kudhibiti uvunaji haramu wa mazao ya misitu katika Hifadhi ya Msitu wa Mazingira asilia wa Chome (Shengena) Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro kwa kutumia ulinzi shirikishi unaohusisha vijiji 27 vinavyoizunguka hifadhi hiyo.



Meneja wa Wakala wa huduma za Misitu Tanzania (TFS)  kanda ya kaskazini Bw. Cuthbert Mafupa akiwaeleza waandishi wa habari(hawapo pichani) waliotembelea hifadhi ya Chome kujionea hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kutunza misitu pamoja na mafanikio yaliyofikiwa katika utunzaji wa hifadhi ya msitu wa Mazingira asilia wa chome (Shengena) ikiwemo kupanda miti katika maeneo yaliyoathika na uvunaji haramu wa rasilimali za msitu huo.

Prof. Vicky Mckinley ambaye ni Mtafiti kutoka chuo Kikuu cha Roosevelt kilichopo Chicago,Illinois  nchini Marekani akipongeza juhudi za Serikali ya Tanzania katika kutunza hifadhi ya Msitu wa mazingira asilia wa Amani uliopo Wilayani Muheza Mkoani Tanga,wakati wa ziara ya Waandishi wa habari katika Msitu huo hivi karibuni.

Msaidizi wa Misitu Mkuu ambaye ni Mkuu wa Kituo cha Zigi katika hifadhi ya Msitu wa asili Amani  bw. Mlega Sossele akiwaeleza waandishi wa habari hawapo pichani jinsi wananchi wanavyonufaika na Msitu huo kwa kuwatengea asilimia 20 ya mapato yanayopatikana kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages