Breaking News

Your Ad Spot

May 28, 2014

Mradi wa jengo jipya la MOI, (MOI Phase III) ambao utagharimu zaidi ya Tshs billion 30 utaisaidia serikali kupunguza gharama za rufaa za kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi kufuata huduma kutokana na baadhi ya huduma na vipimo kutokuwepo nchini,rufaa hizo huwa ni za gharama kubwa sana.

 
Muonekano wa Jengo jipya la Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) ambalo linatarajiwa kukamilika mapema mwaka huu,kukamilika kwa jengo hilo kutasaidia Taasisi hiyo kupanua huduma zake na kupunguza idadi ya wagonjwa wanaoenda kutibiwa nje ya nchi kwa kwa asilimia 80 ikiwa ni juhudi za Serikali kuboresha huduma za Afya hapa nchini.
Meneja Ustawi wa Jamii na Uhusiano wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) Bw. Jumaa Almasi (katikati)akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu hatua iliyofikiwa katika kupanua huduma za Taasisi hiyo ikiwemo kukamilika kwa jengo jipya la kisasa litakalokuwa na vifaa vya kisasa kama MRI ( magnetic Resonance Imaging) CT-SCAN (Computerized Tomography).kushoto ni Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Bi Fatma Salum na kulia ni Afisa uhusiano wa Taasisi hiyo Bw. Patrick Mvungi.Picha zote na Idara ya Habari Maelezo
---
Dar es Salaam, 26/05/2014 Mradi wa jengo jipya la MOI, (MOI Phase III) ambao utagharimu zaidi ya Tshs billion 30 utaisaidia serikali kupunguza gharama za rufaa za kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi kufuata huduma kutokana na  baadhi ya huduma na vipimo kutokuwepo nchini,rufaa hizo huwa  ni za gharama kubwa sana.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages