Breaking News

Your Ad Spot

Jun 2, 2014

KINANA AITEKA MERERALI WILAYANI SIMANJIRI MKOANI MANYARA

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara aliofanya katika Kata ya Mererali, akiwa katika ziara yake ya kukagua uhai wa Chama na Utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia ya kuzitatua katika wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara leo, Juni 2, 2014
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wapili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mchimbaji mdogo, Susie Kennedy (kushoto), alipotembelea machimbo ya wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite, eneo la Mererani, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, leo Juni 2, 2014.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mchimbaji mdogo, Susie Kennedy kuhusu madini ya Tanzanite, alipotembelea machimbo ya wachimbaji wadogo wa madini hayo kwenye machimbo ya Mererani, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, leo Juni 2, 2014. Katikati yao ni Mbunge wa Simanjro, Christopher Ole Sendeka.
 Karibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua tangi la mradi wa maji wa Mererani mkoani Manyara, leo Juni 2, 2014.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakifurahia jambo na mchimbaji mdogo wa Mererani, Mahmoud Karia, baada ya Kinana kuzindua ujenzi wa zahanati katika kata ya Mererani leo, Juni 2, 2014. Picha na Bashir Nkoromo wa theNkoromo Blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages