
Mmoja wa watuhumiwa hao akipakiwa kwenye Gari la Polisi tayari kwa Kupelekwa Mahakamani kusikiliza kesi yao.

Watuhumiwa wakiwa kwenye gari ya Polisi.

Ulinzi Mkali
--
WATU
17 wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu Mkazi jijini
Arusha, kujibu mashitaka 16 yakiwemo ya kuua kwa kutumia bomu,kutesa
binadamu na kusajili vijana na kuwapeleka nje ya nchi kufanya ugaidi.
Watu
hao walifikishwa mahakamani hapo leo na kusomemewa shitaka hilo mbele
ya Hakimu Mkazi Mustafa Siama ambapo hawakutakiwa kujibu chochote
kutokana na kile kilichoelezwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa
kusikiliza kesi hiyo.
Watuhumiwa
hao wanadaiwa kutenda tukio hilo Aprili 13,katika nyumba ya kulala
wageni na baa ya Arusha Night Park iliyopo Mianzini jijini hapa,ambapo
kesi hiyo imeahirishwa hadi juni 11 mwaka huu kwa mtuhumiwa namba moja
na namba nne na watuhumiwa wengine waliobaki kesi yao itatajwa tena Juni
12
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269