Breaking News

Your Ad Spot

Jul 20, 2014

CHADEMA YAZIDI KUTEKETEZWA NA MOTO WA CHAMA KIPYA CHA ACT, TABORA NAKO CHAWAKA

TABORA, Tanzania
WIMBI la viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kukikimbia zimeendea, kufuatia Katibu wa Chama hicho  mkoani Tabora, Othman Balozi na kundi la wanachama wengine kibao kutangaza leo kujiunga na chama kipya cha  ACT Tanzania, ambacho kinaaminika kuasisiwa na aliyekuwa Natibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ambaye kwa sasa amebakia ni mbunge tu kwa tiketi ya chama hicho.

Mbali na Balozi aliyewaongoza wajumbe 78 wa baraza kuu la Chadema hivi karibuni kwenda kwa msajili wa vyama kulalamikia katiba ya Chadema kukiukwa, pia wamo viongozi mbali mbali wa mabaraza ya kimkoa kiwilaya na majimbo walioamua kujitoa na kujiunga na Chama kipya cha ACT-Tanzania

Viongozi hao ni mwenyekiti wa Bavicha mkoa wa  Tabora Hussein Kundecha,mratibu wa uhamasishaji Bavicha  wilaya ya Tabora mjini Nzuki Machibya na Ramadhan Simba Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Bukene.

Wengine ni Suni Yohane aliyewahi kuwa katibu wa Chadema wilaya ya Nzega pamoja na mwenyekiti wa baraza la wanawake katika wilaya hiyo.

Wimbi hilo pia limewazoa wanachama wa kawaida kutoka Chadema na CUF pamoja na watu ambao 200 ambao  hawakuwahi kuwa wanachama wa chama chochote hapo awali.

Kuhama kwa viongozi hao kumekuja ikiwa ni siku moja baada ya waliokuwa viongozi wa Chama hicho mkoa wa Kigoma kubwaga Manyanga

Waliobwaga Manyanga kwa Mkoa wa Kigoma hiyo juzi ni Jafari Kasisiko Mwenyekiti, katibu Msafiri Wamalwa na iti wa Baraza la wanawake wa  mkoa wa Kigoma kubwaga Manyanga

Akizungumzia sababu ya kujiondoa Chadema Balozi alisema kabla ya kufikia uamuzi huo alimpa taarifa mwenyekiti wake wa mkoa Kansa Mbaruku juu ya uamuzi huo

Alisema akiwa miongoni mwa viongozi wa awali kukipokea Chadema katika mkoa wa Tabora,amechoshwa na chama hicho kuacha misingi yake ya  kidemokrasia na kukumbatia Ubabe na dharau huku wakiwanyooshea vidole  vya usaliti wale wanaohoji baadhi ya mambo wasiyoridhika nayo ndani ya Chama hicho.

“Leo mimi ni mtu huru na nimewasikiliza ACT na falsafa yao ya uwazi na kuamua kujinga kwa hiari yangu sasa huu uwazi waudhihirishe na sitasita kuhoji pale penye matatizo nawasihi katika hali hiyo wawe wavumilivu kwa tutakayohoji”alisema Balozi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages