Breaking News

Your Ad Spot

Jul 14, 2014

KOMBE LA DUNIA: BAADHI YA YALIYOJIRI SANJARI NA UJERUMANI KUTWAA KOMBE

WAJERUMANI WALIKABA MPAKA KIVULI CHA LIONEL MESSI, KWA `STAILI` HII KUISOMA NAMBA ILIKUWA LAZIMA TU`!

Star attraction: The World Cup final at the Maracana was the biggest match of Lionel Messi's stellar career
Nyota wa mvuto: Mechi ya fainali ya kombe la dunia katika dimba la Maracana ilikuwa mechi kubwa zaidi katika maisha ya soka ya Lionel Messi.

MCHEZAJI bora wa dunia mara nne mfululizo, Lionel Messi aliibeba Argentina mabegani mwake katika mchezo wa fainali dhidi ya Ujerumani usiku wa leo na kushuhudia nchi yake ikipigwa bao 1-0 na kukosa ubingwa.
Mamilioni ya Waargentina walifurika Rio de Janeiro wakiwa na matumaini makubwa ya kumuona shujaa wao Messi akikata kiu yao ya kutaka ubingwa, lakini mambo yamekwenda ndivyo sivyo. 
Mabeki wa Ujerumani walicheza ngado kwa ngado na Messi na hawakutaka kumuachia hata upenyo.
Marked man: Messi is closed down by three German players and robbed of possession by Bastian Schweinsteiger

Mtu wa kukabwa: Messi alikuwa chini ya ulinzi wa wachezaji watatu wa Ujerumani na mpira ulichukuliwa na kiungo fundi  Bastian Schweinsteiger.
Iconic: The picture of Messi surrounded by Germany defenders was reminiscent of the famous one of Diego Maradona taking on Belgium at the 1982 World Cup. The picture is actually of a fractured defensive wall following a free-kick rather than any concerted pressure on Maradona

Mtu pekee: Picha iliyomuonesha Messi akiwa amezingirwa na wachezaji watatu wa Ujerumani, ilikumbusha enzi za gwiji wa pekee nchini Argentina, Diego Maradona ambaye alikuwa chini ya msitu wa wachezaji wa Ubelgiji katika fainali za mwaka 1982.
Carnage: Messi scrambles for the ball after bursting through the German back line

Messi akichuana kupata mpira baada ya kufanikiwa kuipenya ngome ya ulinzi ya Ujerumani.
Guarded: Messi is surrounded by four German players as he tries to instigate an Argentina attack
Analindwa: Messi akiwa amezingirwa na wachezaji wanne wa Ujerumani , huku akijaribu kutengeneza shambulizi la Argentina.
Not to be: Messi was destined to end up on the losing side as Argentina were beaten 1-0 by Germany after extra time
Haijatimia: Ameshindwa kuandika historia baada ya kushuhudia nchi yake ya Argentina ikipigwa kidude kimoja na Ujerumani.

UJERUMANI BINGWA KOMBE LA DUNIA

Mabingwa 2014: Nahodha wa Ujerumani, Philipp Lahm (wa pili kulia mbele) akinyanyua kombe la dunia na kushangilia .
On top of the world: Germany celebrate as they lift the iconic trophy at the Maracana
Wachezaji wa Ujerumani wakishangilia baada ya kutwaa kombe la dunia katika dimba la Maracana kwa kuifunga Argentina bao 1-0.
The boss: Germany coach Joachim Low (centre) lifts the World Cup as his players celebrate around him
Big Bosi: Kocha wa Ujerumani, Joachim Low (katikati) akinyanyua Kombe la Dunia

LIONEL MESSI AIBUKA KIDUME TUZO YA MCHEZAJI BORA KOMBE LA DUNIA 2014

Scant consolation: Lionel Messi was awarded the Golden Ball trophy for player of the tournament
 Lionel Messi amepewa tuzo ya mchezaji bora wa mashindano .


LICHA ya kupoteza mechi ya fainali na kukosa kombe la dunia mwaka 2014, mshambuliaji wa Argentina na Barcelona, Lionel Messi ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Tuzo hii imekuja kaka ya kustaajabisha kwa watu wengi, lakini kwa kiasi kikubwa alistahili kupewa.
 Messi alionesha kiwango kikubwa katika hatua ya makundi akifunga mabao 4 katika michezo mitatu dhidi ya Bosnia, Iran na Nigeria, lakini nyota yake ilififia baada ya kushindwa kufunga katika mechi za mtoano dhidi ya Switzerland, Ubelgiji, Uholanzi na Ujerumani.
Katika mchezo wa fainali dhidi ya Ujerumani, Messi alipoteza nafasi moja muhimu, lakini muda mwingi alifanya jitihada za kutafuta upenyo bila mafanikio.
Coat of paint: Lionel Messi shoots narrowly wide to miss opening the scoring for Argentina in the Maracana
 Lionel Messi alipiga shuti, lakini alikosa bao katika mchezo wa fainali Maracana.
Baada ya kipyenga cha mwisho, Messi alipokea tuzo yake ya mchezaji bora akiwashinda  nyota wa Colombia James Rodriguez, winga wa Uholanzi, Arjen Robben na wachezaji watatu wa Ujerumani, Manuel Neuer, Bastian Schweinsteiger na Thomas Muller. 
Dream is over: Lionel Messi looks to the ground after Germany win the World Cup at the Maracana
Ndoto zimezima: Lionel Messi akiangalia chini baada ya kupoteza mechi ya fainali dhidi ya Ujerumani.

HISTORIA YA MABINGWA WA KOMBE LA DUNIA TANGU KUANZISHWA

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages