Breaking News

Your Ad Spot

Aug 3, 2014

MANISPAA YA KINONDONI YATAKIWA ISIGAWE KWA UPENDELEO VIZIMBA KITUO KIPYA CHA BIASHARA UBUNGO.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda na Naibu Meya wa Manispaa hiyo, Songoro Mnyonge wakiongoza wajumbe kukagua ujenzi wa Kituo cha Biashara kwa ajili ya Machinga na Mamalishe katika eneo la Kituo Kipya cha Mabasi kinachojengwa nyuma ya jengo la Mawasiliano Tower, Ubungo jijini Dar es Salaam, leo.
 Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akizungumza, wakati wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Kinondoni walipokagua maendeleo ya ujenzi wa eneo la biashara mahsusi kwa machina na Mamalishe, Ubungo
Katibu wa CCM Kinondoni Athumani Shesha akizungumza baada ya ujumbe kukagua
Ujenzi wa kituo hicho cha biashara unaoendeleo

HABARI KAMILI
NA BASHIR NKOROMO
Manispaa ya Kinondoni, imetakiwa kuchukua thabiti kuhakikisha hakuna   upendeleo utakaojitokeza wakati wa kugawa vizimba kwenye eneo la  kisasa la biashara lililojengwa na Manispaa hiyo katika eneo la Ubungo  jijini Dar es Salaam.

Wametaka wakati wa kugawa vizimba kwenye eneo hilo la biashara  lililopo nyuma ya jengo la Masiliano Tower, wapewe kipaumbele  machinga na mamalishe ambao wamekuwa wakitaabika kwa muda  mrefu kutokana na kukosa maeneo ya kufanyia biashara zao katika  Manispaa hiyo.


Hayo yalisemwa jana, kwa nyakati tofauti na Wajumbewa Halmashauri  Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Kinondoni,  walipotembelea eneo hilo la biashara ambalo ni pamoja na mradi wa  Kituo kipya cha daladala kilichojengwa eneo hilo ambacho kinatarajiwa  kuanza kazi mwishoni mwa mwezi huu.


Akijibu angalizo hilo Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda,  alisema, ugawaji huo utasimamiwa na yeye pamoja na wasaidizi wake  wachake na kwamba hakuna upendeleo utakaopenyezwa wakati wa  ugawaji huo.


"Ni kweli kabisa, eneo hilo tunalijenga mahsusi kabisa kwa ajili ya  machinga na mamalishe wa manispaa hii, Wapo watu walishauri tuweke  vitegauchumi mikubwa kama hoteli za kisasa lakini tulikataa, kwa  sababu lengo kubwa na kusaidia walio wengi, kwa hiyo katika ugawaji  vizimba hapa nitasimamia mwenyewe na Msaidizi wangu", alisema  Mwenda.


Mwenda alisema, mradi wa ujenzi wa eneo hilo la biashara ambao  umegharimu sh. bilioni 3, utawanufaisha watu wasiopungua 500 ambao  watakuwa machinga na mamalishe.


Alisema, licha ya akwamba walengwa wakubwa ni machinga na  mamalishe, watu wa kawaida watafikiriwa kupewa vizimba hivyo ingawa  si kwa kipaumbele.


Mwenda alisema, mbali na mradi wa eneo la biashara na kituo cha  kisasa cha mabasi, katika eneo hilo lenye ekari zaidi ya 15, Halmashauri  inajenga pia eneo la huduma za burudani kama lilivyo eneo la Leaders'  Club.


Alisema, pamoja na kujengwa eneo la burudani, pia Manispaa inajenga  katika eneo hilo ukumbi mkubwa wa mikutano ambao utakuwa na  uwezo wa kuchukua watu wengi kwa wakati mmoja ambao utakuwa  tegemeo kubwa kwa shughuli mbalimbali zikiwemo za sherehe kama za  harusi, kongamano na semina.


"Ukisikia mtu anasema CCM haiwapendi wamachinga, Mamalishe na  wananchi wake kwa jumla ni muongo au ana ajenda yake ya siri. CCM  inawapenda hao wote kwa vitendo ndiyo maana Halmashauri yetu ya  Kinondoni kupitia ilani ya CCM imeamua kuwajengea kitu cha aina hii",  alisema Mwenda. HABARI ZAIDI SOMA UHURU KESHO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages