Breaking News

Your Ad Spot

Aug 11, 2014

MBUNGE RIDHIWANI KIKWETE AZINDUA KISIMA CHA MAJI KIJIJI CHA WAFUGAJI CHA MBALA, CHALINZE


 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete akionozana na akina mama wa jamii ya kimasai waliobeba maji waliyoyateka baada ya mbunge huyo kuzindua kisima cha maji katika Kijiji cha Mbala, Chalinze, Bagamoyo mkoani Pwani jana. Kisima hicho pamoja na lambo la kunyweshea mifugo vimejengwa na Kanisa la Wasabato kwa gharama ya sh. mil. 76. Kushoto ni Kiongozi wa mradi huo, Joseph Chagama na nyuma yake ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
 Ridhiwani Kikwete akifunua pazia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kisima hicho. Kushoto ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana.
 Ridhiwani akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa jamii ya kimasai baada ya kuzindua kisima hicho.
 Mama mwingine wa Jamii ya Kimasai akitwisha ndoo ya maji na Ridhiwani Kikwete

 Ridhiwani Kikwete akifungua maji ikiwa ni ishara ya kuzindua lambo la kunyweshea mifugo katika Kijiji cha Mbala kinachokaliwa kwa asilimia kubwa na jamii ya wafugaji
 Ng'ombe wakitoka kunywa maji kwenye lambo hilo
 Watoto wa kimasai waonja maji ya kwenye lambo baada ya uzinduzi
 Kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Wasabato la Mbala, ikitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa kisima cha maji uliofanywa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, katika Kijiji cha Mbala, Chalinze, mkoani Pwani jana. Kanisa hilo limejengwa na Kanisa la Wasabato kwa gharama ya sh. mil. 76. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Ridhiwani Kikwete (wa pili kulia) akishiriki katika maombezi
Kwaya ya Kanisa la Wasabato la Manzese wakimwimbia bwana wakati wa hafla hiyo

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages