Breaking News

Your Ad Spot

Sep 24, 2014

KINANA AKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA KUSHIRIKI KAZI ZA MAENDELEO WILAYANI KILINDI

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi, bada ya kuwasili Kata ya Kwediboma, wakati akiingia mkoa wa Kilindi kutoka wilaya ya Handeni, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCm katika mkoa wa Tanga, leo, Septemba 24, 2014.
 Wazee wa Kilindi wakimsubiri kwa hamu Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati wa mapokezi yaliyofanyika, Kijiji cha Kwediboma, wilayani humo, Septemba 24, 2014.
Umati wa wananchi wa Kwediboma, wakiwa wamekusanyika kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alipozungumza nao kabla ya kushiriki ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kwediboma, leo Septemba 24, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika mkoa wa Tanga.


 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa Kituo cha Afya,  leo Septemba 24, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika mkoa wa Tanga.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akibeba ndoo za zege, wakati akishiriki ujenzi wa jengo la Kituo cha Afya cha Kijiji cha Kwediboma, leo Septemba 24, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika mkoa wa Tanga.
Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana akimwaga zege, aliposhiriki ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kwediboma,  leo Septemba 24, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika mkoa wa Tanga.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana aakiwasalimia wananchi baada ya kuwasili Kata ya Kibirashi, kushiriki ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari ya Kata hiyo, leo Septemba 24, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika mkoa wa Tanga.
Kinamama wa Kibirashi wakimshangilia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alipowsili kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji hicho,  leo Septemba 24, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika mkoa wa Tanga.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, uliofanyika katika kijiji cha Kibirashi, wilaya ya Kilindi mkoa wa Tanga, leo Septemba, 24, 2014.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kibirashi, wilaya ya Kilindi mkoa wa Tanga, leo Septemba, 24, 2014. (Picha zote na Bashir Nkoromo)
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kulakiapo na wanachama wapya wa CCM waliokuwa wakiapishwa baada ya kuwakabidhi kadi za CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kibirashi, wilaya ya Kilindi mkoa wa Tanga, leo Septemba, 24, 2014. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages