Hii ndio filamu mpya ya 990 wamekufa inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni na wasanii wa Miale sanaa Group wa Iringa |
Mkurugenzi mtendaji wa Miale sanaa Group Bw Nurdin Khamis kushoto wa kwanza akiwa na baadhi ya wasanii wanaounda kundi hilo |
Mkurugenzi mtendaji wa Miale sanaa Group Bw Nurdin Khamis akihojiwa
Akizungumza
na mtandao wa matukiodaima.co.tz mkurugenzi mtendaji wa kundi hilo
Nurdini Khamis alisema kuwa kundi hilo limeendelea kufanya vema
katika tasnia ya filamu nchini kutokana na wasanii wake kuifanya
kazi hiyo kwa kutumia vipaji halisi vya kuzaliwa na hivyo kuwa
tofauti na wasanii wengine ambao wamekuwa wakiifanya kazi hiyo
kwa kutegemea elimu ya vyuo vya sanaa.
Na MatukiodaimaBlog
WASANII
wasanii wa Miaele sanaa Group wa mjini Iringa mkoani Iringa waanza
kutembeza bakuli kuomba kuchangia kiasi cha Tsh milioni 3 kwa ajili ya
kukamilisha uzinduzi wa filamu yao mpya ya 990 wamekufa .
Alisema
kuwa kuanzishwa kwa kundi hilo ni jitihada zake binafsi baada ya
kuona mkoa wa Iringa una wasanii wenye uwezo wa kuigiza ila hakuna
sehemu ya kuonyesha vipaji vyao na ndipo alipoanzisha kundi hilo
mwaka 2009 kwa kuwa na wasanii 30 kabla ya kufanyiwa mchujo .
Khamis
alisema kuwa mara baada ya mazoezi makali zaidi wale ambao
walifanyiwa mchujo waliweza kuonyesha uwezo mkubwa katika uigizaji
na hivyo kulazimika kutoa kazi yao ya kwanza iliyokwenda kwa jina
la Zero Done kwa kuwashirikisha wasanii wakubwa nchini kama Senga ,
Mwamba , Mzee Pembe , Patcho ,Halima Madiwa , Rado na wengine wengi
wenye majina makubwa kazi ambayo ilisambazwa nchi nzima na
kuonyesha kupendwa zaidi.
Aidha
alisema kutoka na ukata wa fedha wameendelea kufanya kazi hiyo
kwa kusua sua japo kwa sasa wanataraji kuibuka na filamu kali
kuliko ya 990 wamekufa ambayo inategemewa kuzinduliwa wakati
wowote kuanzia sasa mara baada ya maandalizi kukamilika.
Mkurugenzi
huyo alisema kuwa kutokanana na uwezo mdogo wa kipato na aina ya
wasanii wanaounda kundi hilo kutokuwa na kazi za kufanya kundi hilo
limeendelea kuwa tegemezi zaidi kwa kufanya kazi kwa migongo ya
wafadhili mbali mbali na kuwa hata filamu hiyo iliyopo jikoni
inategemea kuzinduliwa kwa ufadhili wa kamanda wa UVCCM mkoa Salim
Asas , Jackson Kiswaga ambae ni mkazi wa Iringa na mdau wa sanaa katika
mkoa wa Iringa aliyechangia kiasi cha Tsh 500,000
Pamoja
na kuwashukuru wadau mbali mbali kwa kuendelea kujitolea kusaidia
ukuaji wa tasnia ya sanaa katika mkoa wa Iringa bado alisema kuwa ni
mategemeo yao kuwa wadau hao wataendelea kutoa ushirikiano zaidi
kwao ili kufanikisha kuutangaza zaidi mkoa wa Iringa kisanaa
kutokana na uwezo mkubwa wa wasanii wanaounda kundi hilo.
Kwani
alisema mipango ya mbeleni kwa kupitia kundi hilo kuanzisha
utaratibu wa kutengeneza filamu za kuelimisha jamii juu ya masuala
mbali mbali ya kimaendeleo katika mkoa wa Iringa na Taifa kwa ujumla
ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya kulinda hifadhi zetu kutoingiliwa
na majangili .
Hivyo
aliomba wale wote wenye mapenzi ya dhati na kundi hilo kujitokeza
kuchangia chochote kwa kupitia huduma ya M- Pesa kwa namba 0757 698
582 kwa madai kuwa bila kusaidiwa na wadau mbali mbali uwezo wao
ni mdogo zaidi kiuchumi ila kisanaa wapo juu ukilinganisha na makundi
mengine makubwa nchini.
"
Uwezo wa kucheza filamu zenye ubora tunao na ndio maana vituo
mbali mbali vikubwa vya runinga ikiwemo Zuku swahili wamekuwa
wakirusha kazi zetu baada ya kuona ni bora zaidi"
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269