Baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar wakiingia katika Viwanja vya Mahafali chuoni hapo.
Mgeni
Rasmi Waziri wa Fedha wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Saada Mkuya katikati mwenye miwani akiwa katika Picha ya pamoja na
viongozi wachuo na Wahitimu wa mahafali ya sita ya Chuo cha Maendeleo ya
Utalii Zanzibar. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar). Baadhi
ya Wahitimu wa Fani ya Upishi wakiwa wanamsikiliza Mgeni Rasmi Waziri
wa Fedha wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Saada Mkuya
hayupo pichani wakati wa sherehe ya Mahafali ya Sita ya Chuoni hapo. Baadhi
ya Wahitimu wa Fani ya Ukarimu na Uongozi wa Hoteli wakivaa kofia
kuashiria kukabidhiwa Stashahada zao katika Mahafali ya sita ya Chuo cha
Maendeleo ya Utalii Zanzibar Mwanafunzi
Bora Chuoni hapo wa Fani ya Mapokezi ya Wageni “Front Office”Said
Shaame Khamis akipokea Zawadi kutoka kwa Mgeni Rasmi Waziri wa fedha wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Saada Mkuya katika Mahafali
hayo Yaliyofanyika Maruhubi mjini Zanzibar
……………………………………………………………
Na Faki Mjaka- Maelezo Zanzibar
Waziri wa Fedha wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Saada Mkuya amewataka Wahitimu wa Chuo
cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar kutoitegemea Serikali katika kupata
ajira badala yake wajikite katika kujiajiri wenyewe.
Amesema nafasi za Ajira Serikalini
ni chache hivyo Wahitimu hao wanapaswa kujishughulisha ili wajiajiri
wenyewe au kupitia Taasisi Binafsi.
Waziri Mkuya ameyasema hayo
alipokuwa akitoa hutuba yake kwa Wahitimu wa Mahafali ya Sita ya Chuo
cha Maendeleo ya Utalii yaliyofanyika leo kati viwanja vya Chuo hicho
Maruhubi Mjini Zanzibar.
Amesema dhana ya kuitegemea
Serikali katika ajira kwa sasa haina nafasi kutokana na uchache wa Ajira
na kwamba anaamini Elimu waliyoipata Wahitimu inaweza kuwasaidia katika
kujiajiri.
Ametoa Rai kwa Wahitimu hao
kujiunga na Kampuni za Ulinzi ambazo zinatarajiwa kuanzishwa Zanzibar
kutokana na kuripotiwa kwa matukio mbalimbali ya kihalifu nchini.
Aidha Waziri Mkuya amewashauri
Wahitimu hao kutotosheka na kiwango cha Elimu walichofikia badala yake
wajiendeleze mbele ili kupata ufanisi katika kazi zao.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chuo
hicho Bi Zulekha Khamis Omar amesema Chuo hicho kinazidi kupiga hatua
kimaendeleo nakwamba Wanatarajia kuanzisha Masomo ya Shahada ya Kwanza
mwaka 2017-18.
Amesema mipango ipo mbioni
kukamilika kuhusu kuanzishwa kwa Masomo ya Shahada ambapo Chuo hicho
kitakuwa Chini ya Chuo Kikuu cha Zanzibar SUZA
Hata hivyo Bi Zulekha alizitaja
Changamoto zinazokabili Chuo hicho kuwa ni pamoja na Uhaba wa Vifaa
katika Jiko, na Mmommonyoko wa Ardhi unaotishia Mazingira ya Chuo hicho.
Chuo hicho kilichoanzishwa mwaka
1992 ili kuongeza ukuaji na Maendeleo ya Utalii Zanzibar kimefanya
Mahafali yake ya sita ambapo Jumla ya Wahitimu 511 wa Ngazi za
Stashahada na Cheti katika Fani mbalimbali wamehitimu.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269