Diamond
Platnumz ni miongoni mwa marafiki wa karibu wa msanii Dully Sykes
ambaye weekend iliyopita alimpoteza baba yake mzazi Ebby Sykes, lakini
hakuweza kuhudhuria msiba huo kutokana na sababu ambazo amezitoa leo.
Diamond
ambaye wakati msiba huo unatokea alikuwa Zanzibar na mpenzi wake Zari,
ameelezea sababu zilizomfanya kushindwa kuhudhuria mazishi.
“Watu waliniona niko zanzibar lakini walikuwa hawajui nimeenda kufanya nini,” Diamond ameiambia 255 ya XXL ya Clouds FM. “Usiangalie
kila unachokiona Instagram ukajua mtu labda kwasababu alikuwa anafanya
starehe. Niko katika kipindi ambacho sio kizuri kwangu mimi na familia
yangu kwasababu kuna vitu ambavyo siwezi kuvizungumza lakini, na siwezi
kuviweka kwenye media ndo maana watu wengine wanaweza kuniona nacheka
lakini […] kwanza mama yangu anaumwa na anaumwa sana sijawahi
kulizungumza hili ndo nalizungumza hapa, hapa ninapoongea na wewe yupo
India, kuna vitu vingi vinaendelea, siwezi kusema nilikuwa Zanzibar
nafanya nini, inawezekana ikawa ndo sababu iliyonifanya mpaka mimi
nikachelewa kwenda kwenye msiba, lakini inawezekana labda mimi ndio
nilikuwa mtu wa kwanza kutoa pole katika social networks zangu mimi.”
“Unajua wakati mwingine ni vizuri kwenda kuzika lakini inawezekana mtu
akawa ameenda kuzika lakini mi nikawa sijaenda kuzika nikawa nimefanya
kitu cha maana kuliko wale walioenda kuzika kwasababu huwezi kujua
nilifanya kitu gani. Nilisikia niliambiwa watu walikuwa wanongea sijui
Diamond hajafika lakini naamini kuna watu wengi hawakufika na kila mtu
hakufika kwa sababu fulani. Dully mi ni kama kaka yangu kabisa ni mtu
ambaye amenisaidia vitu vingi sana isingewezekana kabisa niko ninanafasi
nishindwe kwenda kwenye msiba.”
“Ukiacha
tu Dully mwenyewe kwanza mtu aliyefariki ni kama mzee wangu, na mtu
ambaye amefanya kitu kikubwa katika sanaa hii ya muziki na mimi nimefika
hapa yeye pia ana mchango wake, so haikuwa rahisi eti mimi nisiende tu
nikiwa sina sababu, kulikuwa na sababu na ndio maana.” Alimaliza Diamond.
~Bongo5
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269