Breaking News

Your Ad Spot

Feb 26, 2015

FILIKUNJOMBE AWATAKA MAWAZIRI WAACHE KULALAMIKA

Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe. 

Na Francis Godwin, Njombe
MBUNGE wa jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe (pichani), amewavaa Mawaziri walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kutoka Mkoa wa Njombe kwa kushindwa kusaidia ukuaji wa mkoa huo, na badala yake kuwa mawaziri wa kulalamika tu.

Mbunge Filikunjombe aliwavaa Mawaziri hao leo, baada ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Rehema Nchimbi kuwapa nafasi Mawaziri na Mbunge huyo kama wajumbe wa juu wa kikoa cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC), ili kuchangia juu ya namna ambavyo Mkoa wa Njombe unaweza kupata kiasi cha Tsh zaidi ya bilioni 158.6 kwa ajili ya bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016.
Wakati mawaziri wawili akiwemo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Dr Binilith Mahenge na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Pindi Chana wakitaka watumishi wa umma kuwajibika vema katika ukusanyaji wa mapato.
Waziri Dk Pindi ambaye ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Njombe akichangia alisema ni suala la Halmashauri kujitathimini kwani ni jambo na kujiuliza kwa halmashauri kujipangia makusanyo na kushindwa kutimiza malengo yake .

Huku waziri Dk. Mahenge ambae ni mbunge wa jimbo la Makete akiutaka mkoa kuwabana wakuu wa idara kuwa na matumizi mazuri ya fedha kwa kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha za umma badala ya kuwa na matumizi mabaya pia kuangalia uwezekano wa kutupunga watumishi wasio na tija katika Halmashauri .

Blioni 9 zinategemewa kukusanywa katika mkoa wa Njombe kwa mwaka wa fedha 2015/2016 huku mkoa huo ukiomba maalum ya kuhidhinishiwa kiasi cha zaidi ya Tsh bilioni 158.6 kwa ajili ya uendeshaji wa mkoa kwa maana ya kulipa mishahara ya watumishi ,miradi ya kimaendeleo na matumizi mengine.
Kwa upande wake mbunge wa Ludewa Bw Filikunjombe akichangia juu ya mkakati huo wa uopatikanaji wa kiasi hicho cha fedha za uendeshaji wa mkoa alisema kuwa kwa upande wake asingependa kuchangia suala hilo kwani wapo mawaziri katika mkoa wa Njombe ambao ndio wapo jikoni hivyo ni matumaini yake kusikia majibu yao badala ya kuishia kulalamika.
Mbunge Filikunjombe akichangia katika kikao cha RCC Njombe.
Mjumbe wa kikao cha RCC alikuwa akichangia jinsi ambavyo Serikali Kuu inavyokwamisha maendeleo wilayani.

"Kweli mimi mheshimiwa mwenyekiti kunitaka niseme hapa ni kunionea kwani humu ndani katika kikao chetu tunao vijana wetu ambao ni mawaziri sasa ni vema wao kusema zaidi na sio kuishia kulalamika....maoni yangu binafsi haya ni maoni yangu binafsi sana .....mimi ningependa sana kila mmoja kutimiza wajibu wake serikali itimize wajibu wake wabunge na watendaji pia hivyo hivyo.... kuna shida hapa tunapanga mambo tunawapangia hadi wahisani halafu baadae tunaanza kulalamika".
Mbunge Filikunjombe aliwataka watendaji serikali kuacha kuwa walalamikaji na badala yake kila mmoja kutimiza wajibu wake kwa pale walipo.

Alisema kuwa ilipendeza mawaziri hao ambao ndio serikali kuu kuzipongeza Halmashauri za mkoa wa Njombe kwa kufanikisha kukusanya mapato kwa asilimia 40 badala ya kutoa majibu ya kulalamika huku Halmashauri hizo zikiendelea kuidai serikali kuu pesa zao za ushuru wa mazao zaidi ya mamilioni bila kulipa kwa wakati.

Hivyo alisema kwa kuwa wapo vijana ndani ya serikali kuu ni ukombozi wa Halmashauri za mkoa wa Njombe zinazoidai Serikali Kuu.
katika hatua nyingine mbunge Filikunjombe alieleza kusikitishwa baadhi ya watu wanaotaka nafasi za uongozi na biashara kwa kutumia viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) na kumtaka mkuu wa mkoa wa Njombe kuandika barua katika taasisi zote za dini na vyama vya siasa ili kusaidia kukemea suala hilo kabla ya kuingia mkoani hapo.

Alisema kuwa imekuwa ikisikika katika mikoa mingine mauaji na ukatili wa kutisha japo katika mkoa wa Njombe suala hilo bado hivyo ni vema kulithibiti mapema .

Wakati waziri Dr Pindi akiungana na kupinga ukatili wa adhabu ya viboko zaidi ya vitatu kwa wanafunzi nchini pamoja na kukemea tabia ya baadhi ya wazazi wanaowafundisha watoto wao wa kike masuala ya uzazi wa mpango kuwa suala hili halina budi kukomeshwa mara moja.

Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa Dr Nchimbi alikubaliana na ushauri wa Filikunjombe wa kuandika barua kwa taasisi mbali mbali zikiwemo za dini ili kusaidia kutoa elimu juu ya ukatili mkoani Njombe.
wakati huo huo mkuu huyo wa mkoa wa Njombe Dk. Nchimbi ameagiza wanafunzi wa shule za msingi katika kukabiliana na hali ya baridi mkoani humo kuanza kuvaa sare ya suruali badala ya kaptula kama ilivyoagizwa na wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi.
Alisema kuwa kutokana na hali ya hewa ya baridi kali mkoa wa Njombe ni vema viongozi mkoani hapa kuangalia uwezekana na kufanya mabadiliko ya sare hizo za wanafunzi ili kuvaa suruali.
Alisema kuwa hali ya hewa ya mkoa wa Njombe ni hali ya baridi kali hivyo kuna haja ya wanafunzi hao kulinda kiafya zaidi kwa kubadilishiwa sare hizo ili kuvaa suruali kwa ajili ya kujisitili na baridi kali.
"Ndugu wajumbe mkoa wetu ni mkoa wenye baridi kali hivyo kuendelea kuwaacha watoto wetu kutumia sare hizi za kaptula ni kuwatesa zaidi ......naona si vibaya kubadili sare na wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi kuelezwa sababu hii mbona wanaume wa Njombe kutokana na baridi hii wanavaa suruali tena wengine wanavaa mbili zaidi sasa iweje watoto wetu kuendelea kuteseka na baridi"alisema

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa alitaka viongozi wa mkoa wa Njombe kuwa na jibu moja kwa swali la ujenzi wa maabara na uhaba wa madawati kwa kila wanapoulizwa waseme wamekamilisha ujenzi huo wa maabara mbali ya kuwa wamekarabati vyumba vya madarasa yaliyokuwepo.

" Naomba tuwekane sawa hapa kuna vijimaneno maneno vimeanza kusikika kuwa hatujakamilisha ujenzi wa maabara ukweli sisi tumetumia mbinu zetu kukamilisha maabara kama tumegeuza vyumba vya madarasa hiyo ni mbinu yetu wao walitaka maabara na maabara zote zipo na sisi hatuna upungufu wa vyumba vya madarasa wala maabara"

Wakati huo huo serikali ya mkoa wa Njombe imewataka viongozi wanaohusika na migao ya fedha za uondeshaji wa mikoa kuutazama mkoa wa Njombe kwa jicho la tatu ili mgao wake uwe mkubwa zaidi kama njia ya kuuwezesha mkoa huo kusonga mbele mbele kimaendeleo.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Dk. Nchimbi alisema kimsingi mtoto ndie anayepata mahitaji bora ili apate kukua hivyo mkoa wa Njombe wenye utajiri mkubwa wa chuma na makaa ya mawe unahitaji kutengewa bajeti kubwa zaidi ili kuweza kupita hatua na kuweza kuwa mkoa wa kiuchumi kwa Taifa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages