IVORY COAST YAFANYA MAUAJI MATAIFA HURU AFRIKA!
Timu
ya taifa ya Ivory Coast imekuwa timu ya nne kufuzu hatua ya nusu
fainali ya michuano ya kombe la mataifa ya Afrika baada ya kushinda
mchezo wao dhidi ya timu ya taifa ya Algeria .
Ivory Coast imeifunga Algeria kwa matokeo ya 3-1 katika mchezo ambao ulimalizika ndani ya dakika 90 .
Mabao ya Ivory yalifungwa na Wilfred Bony ambaye alifunga mabao mawili huku Gervinho akifunga bao moja .
Bao pekee la Algeria lilifungwa na Hilal Soudani kwenye kipindi cha pili .
Kwa matokeo haya Ivory Coast watacheza nusu fainali na Congo Drc huku
Ghana wakicheza nusu fainali na wenyeji wa michuano hii Equatorial
Guinea
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269