Watu
wanawapenda mastaa, wapo wanaowapenda mpaka wanatamani wafanane nao,
mara nyingi tumekutana na hizi story za watu ambao wamekuwa wakifanya
majaribio ya kujibadilisha muonekano, maumbile yani ili tu afanane na
staa wake anayempenda.
Jordan James alitumia dola 150,000 (zaidi ya mil 270/-) ili kujibadilisha afanane na Kim Kardashian, safari hii ni Adam Guerra ambaye yeye jitihada zake alikuwa akizifanya ili afanane na Madonna.
Pesa
aliyotumia ni paundi 75,000/- (sawa na mil. 210/-) na kutokana na
‘ukarabati’ ambao anataka kuendelea kuufanya kwenye mwili wake mpaka
zoezi likamilike kiasi cha pesa kitakuwa kimefikia paundi 100,000/-
Adam anasema anavutiwa sana na Madonna ndio maana anafanya kila kitu ili afanane naye.
“Nimewahi
kupanda jukwaani nikamuiga Madonna.. nilipata mashabiki wengi, nimekuwa
nikivutiwa naye kwa kila kitu, nimefanya maamuzi yangu binafsi kwa
kutumia hela zangu ili nifanane naye kutokana na mapenzi yangu kwake,
pia nimepanga kufanya ziara za kimataifa ili kuwadhihirishia watu jinsi
gani navutiwa naye“-Guerra
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269