Breaking News

Your Ad Spot

Feb 28, 2015

SIMBA SI SIFA HIYO KUICHAPA TANZANIA PRISONSMABAO 5-0 LIGI KUU VODA COM UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM

Wachezaji wa timu ya Simba wakitoka kushangilia moja ya bao lao waliloifungia timu yao hiyo dhidi ya Tanzania Prison ya Mbeya, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo. Simba imeshinda mabao 5-0. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) 
Wachezaji wakishangilia moja ya bao lao, waliloifungia timu yao hiyo dhidi ya Tanzania Prison ya Mbeya, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo. 
Ibrahim Ajib (kulia) wa Simba akipambana na wachezaji wa timu ya Prison wakati wa mchezo huo.
Ibrahim Ajib (kulia) wa Simba akipambana na Nurdin Chona wa timu ya Prison wakati wa mchezo huo.
Ibrahim Ajib (kulia) wa Simba, mfungaji wa mabao 3 ya Simba (Hat Trick), akiwania mpira na Nurdin Chona wa timu ya Prison wakati wa mchezo huo.
Nurdin Chona wa timu ya Prison, akimtoka Ibrahim Ajib wa Simba. 
Nurdin Chona wa timu ya Prison (kushoto), akiwania mpira na Ibrahim Ajib wa Simba.
Dan Sserunkuma wa Simba, akijaribu kumpiga chenga Nurdin Chona wa Prison.
Dan Sserunkuma wa Simba, akimtoka Nurdin Chona wa Prison. 
Emmanuel Okwi wa Simba, akimtoka James Mwasote wa Prison. 
Mashabiki wa Simba wakifuatilia mchezo huo. 
Wachezaji wa Simba wakishangilia moja ya mabao yao, waliyoifunga timu hiyo, ya Prison.
Wachezaji wa Simba wakipongezana baada ya kupata bao katika mchezo huo.  
Mashabiki wa Tanzania Prison wakizozana baada ya timu yao kufungwa mabao 5-0 na Simba katika mchezo huo. 
Emmanuel Okwi wa Simba, akijaribu kumpiga chenga Nahodha wa timu ya Prison. 
Emmanuel Okwi wa Simba, Nahodha wa timu ya Prison, wakikimbilia mpira.  
Emmanuel Okwi (kushoto), akimpongeza Ramadhan Singano 'Messi' baada ya kuifungia timu yake bao la nne katika mchezo huo. 
Ramadhan Singano 'Messi' (akisujudu), baada ya kuifungia timu yake bao la nne katika mchezo huo, huku wenzake wakimuangalia. 
Ramadhani Singano, akisherehekea bao lake, aliloifungia timu yake hiyo kwa kusujudi huku mwenzake Mohamed Hussein akimnyanyua kwa ajili ya kwenda kuendelea na mchezo dhidi ya Prisons.
Ibrahim Ajib, akiwa na mpira wake aliokabidhiwa baada ya kuifungia timu yake mabao 3 (Hat Trick), katika mchezo huo. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages