Ligi
Kuu Tanzania bara imeendelea leo katika viwanja vitatu tofauti ambapo
Mtibwa Sugar imeendelea kulia baada ya kufungwa na Mgambo bao 1-0
katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Bao la Mgambo limefungwa na Malimi Busungu dakika ya 27.
Kwa
matokeo hayo sasa Mgambo imefikisha pointi 17 na kupanda hadi nafasi ya
12 wakati Mtibwa ikibaki na point zake 19 katika nafasi ya 6.
Ndanda FC ya Mtwara nayo imewachapa Wagosi wa Kaya timu ya Coastal Union
kutoka jijini Tanga bao 1-0 katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la
Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Ndanda imefikisha point 19 na kupaa hadi nafasi ya 10 wakati Coastal ambayo nayo ina point 19 ikibaki nafasi ya 7.
Huko Shinyanga wakata miwa wa Kagera Sugar wameendelea kuutumia uwanja
wa Kambarage kwa mafaniko ambapo leo wamepata ushindi wao wa 3 mfululizo
kwa kuwapiga Maafande wa Jeshi la Polisi kutoka mjini Morogoro bao 1-0.
Bao la Kagera limefungwa kunako dakika ya 38 na Rashid Bunda na kuifanya
Kagera ifikishe point 24 katika nafasi ya Tatu ikiwa ni point mbili
nyuma ya Azam FC.
Polisi Morogoro wamebaki na point zao 19 katika nafasi ya 9.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumapili katika viwanja vitatu tofauti,
Uwanja wa Chamazi wenyeji Azam FC wataikaribisha timu ya maafande wa
Jeshi la Magereza nchini Tanzania Prisons, mchezo utakaonza majira ya
saa 2 kamili usiku.
Mjini Shinyanga wenyeji timu ya Stand United wataikaribisha Simba SC
kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku wagonga nyundo wa jiji
la Mbeya, timu ya Mbeya City wakicheza na timu ya Young Africans kwenye
Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269