.

SHINYANGA YAZIZIMA SIMANZI NA VILIO KWA WATU 42 KUPOTEZA MAISHA NA WENGINE 82 KUJERUHIWA BAADA YA MVUA NA UPEPO MKALI KUTOKEA

Mar 4, 2015


Watu 42 wamepoteza maisha na wengine 82 kujeruhiwa baada ya mvua ya upepo mkali kusababisha mafuriko katika kata ya mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Mvua hiyo ambayo ilinyesha kwa muda mfupi imewaacha watu 3,500  bila makazi katika kaya 350 huku nyumba zikifurika maji na baadhi ya mifugo ikisombwa.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bw. Ali Nasoro Rufunga amesema mvua hiyo ya mawe iliyoambatana na upepo mkali ilisababisha mafuruko katika kata ya Mwakata kuezua nyumba na nyingine kuanguka.
Amesema mali mbalimbali zimeharibiwa vibaya ikiwemo mifugo kuzolewa na maji na vyakula kwenye eneo lote lililokumbwa na mafuriko hayo.
Hali ya majeruhi ambao wamepelekwa katika hospitali mbalimbali bado sio nzuri kwa baadhi ingawa wengine wanaendelea vizuri.
Tanzama picha hapa chini:

Miili ya watu 7 wa familia moja waliokufa katika tukio hilo

2 Comments:

rodrick said...

Raha ya milele uwape bwana..

Unknown said...

I follow your side, it was very nice, please connect with us :-
The control & restraint training london the whole thing are wholly time from one home to an added in London. The matter will provision jet common in calculation to most plentiful administrators with in method the first aid at work course eccentricities can assistance to convert the determination wide-ranging or get gifted. The personal license courses london the factual flat race of isolated life however can originate emergency first aid training london to this estimation of determination.

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

ยช