Breaking News

Your Ad Spot

Mar 26, 2015

WAZIRI LUKUVI AANZA ZIARA MKOANI RUKWA

1
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Injinia Stella Manyanya alipowasili uwanja wa ndege wa Sumbawanga kuanza ziara ya kutatua migogoro ya ardhi Mkoani humo.
New Picture (7)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akimpokea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipowasili eneo la Jangwani mjini Sumbawanga kuweka jiwe la msingi katika nyumba za makazi zinazojengwa na NHC kwa ajili ya kuuzia wananchi.
New Picture (1)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akisalimiana na Kamishna msaidizi wa ardhi kanda ya nyanda za juu kusini Bw. Msigwa mara alipowasili Mkoani Rukwa kutatua migogoro ya ardhi.
New Picture (5)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akitoa msimamo wa dhati wa serikali (kwa wananchi waliofurika kumsikiliza hawapo pichani) wenye nia ya kutatua mgogoro wa ardhi uliopo kati ya mwekezaji na wananchi wa vijiji vya Skaungu na Mawensuzi alipofika katika eneo la Malonje Wilayani Sumbawanga.
New Picture (12)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akihutubia halaiki ya wananchi waliohudhuria sherehe za uwekaji jiwe la msingi kwenye nyumba za makazi zinazojengwa na NHC eneo la Jangwani Mkoani Rukwa. Alisisitiza Halmashauri nchini kutenga ardhi kwa ajili ya NHC kujenga nyumba za gharama nafuu.
New Picture (11)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akitoa maelezo ya mradi wa nyumba za makazi zinazojengwa na NHC eneo la Jangwani mjini Sumbawanga kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi (hayupo pichani) jana.
New Picture (13)
Mbunge wa Sumbawanga Mhe. Hilal Aeshi akiishukuru NHC kwa kujenga nyumba za makazi eneo la Jangwani kwa ajili ya kuuzia wananchi.
New Picture (4)
Mwenyekiti wa kijiji cha Skaungu Bw. Pascal Mwanakatwe akisoma risala kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi kuelezea mgogoro wa ardhi unaokabili kijiji hicho na mwekezaji kanisa la Efatha baada ya Waziri Lukuvi kufika eneo la Malonje kuwasikiliza wananchi ili serikali ipate mwelekeo wa kutatua mgogoro huo.
New Picture (2)
Watendaji wa sekta ya ardhi wakiratibu mazungumzo ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipozungumza na watendaji wa Mkoa wa Rukwa (hawapo pichani ) juu ya migogoro ya ardhi inayowasumbua wananchi.
New Picture (3)
Wananchi wa kijiji cha Skaungu wakimsikiliza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipofika kijiji kilichopo kilomita 50 kutoka mjini Sumbawanga kueleza nia ya serikali ya kumaliza mgogoro wa wananchi na Kanisa la Efatha ambalo ni mwekezaji na mmiliki wa mashamba yanayolalamikiwa na wananchi na kukisababisha mauaji ya mara kwa mara.
New Picture (9)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akiweka rasmi jiwe la msingi katika nyumba za makazi zinazojengwa na NHC eneo la Jangwani mjini Sumbawanga kwa ajili ya kuuzia wananchi. Nyumba hizo zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni mwaka huu.
New Picture (8)
Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC Bw. Haikamen Mlekio akitoa maelezo ya ujenzi unaofanyika eneo la Jangwani kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipowasili kuweka jiwe la msingi la nyumba hizo jana.
New Picture (6)
Kikundi cha ngoma za kifipa kikiburudisha wananchi waliohudhuria sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi nyumba za makazi zinazojengwa na NHC eneo la Jangwani Sumbawanga muda mfupi kabla ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi kuwasili eneo hilo.
New Picture (14)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akisikiliza na kupokea barua za malalamiko ya wananchi waliofurika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa jana ili kuwasilisha kero zao za ardhi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages