Askari
mmoja wa jeshi la polisi ambao hutumia pikipiki kufanya doria,
aliyejulikana kwa jina la Ramadhani, ameuawa mchana huu na wananchi
wenye hasira mjini Morogoro kwa kutuhumiwa kusababisha ajali ya dereva
wa bodaboda ambaye aliparamia lori.
Tukio
hilo linawahusisha askari wawili wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU)
waliokuwa wakiendesha pikipiki yenye namba za usajili za PT 823 ambayo
ni mali ya polisi.
Mashuhuda
wamesema kwamba polisi hao walikuwa wakimfukuza dereva huyo wa bodaboda
ambaye alikwenda kujikita katika lori ambapo wananchi waliwatuhumu
kusababisha ajali hiyo na kuanza kuwashambulia.
Baada
ya kuona hivyo, polisi hao walianza kurusha risasi hewani lakini
wananchi waliwakabili kwa kuwarushia mawe na hivyo kumwua polisi mmoja
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269