Hatimaye
wanafunzi wa zamani wa kocha wa Manchester United – Louis Van Gaal,
katika klabu ya FC Barcelona watapata nafasi ya kuonyeshana umwamba
katika kuelekea jijini Berlin Ujerumani ambapo fainali ya ligi ya
mabingwa wa ulaya itachezwa.
Ratiba ya nusu fainali ya michuano hiyo imepangwa muda mfupi uliopita, huko Nyon – Uswiss.
Ratiba
inaonyesha Luis Enrique ataiongoza FC Barcelona kukipiga dhidi ya FC
Bayern Munich inayofundishwa na mchezaji mwenzie wa zamani wa Barca –
Pep Guardiola.
Guardiola na Luis Enrique walikuwa kwenye kikosi kimoja cha Barca kilichokuwa kikifundishwa na Van Gaal msimu wa 1999/2000.
Kwa
upande mwingine mabingwa watetezi wa kombe hilo, Real Madrid watacheza
dhidi ya Juventus. Mechi za raundi ya kwanza zitachezwa Mei 5 na 6 na
marudiano zitakuwa wiki moja itakayofuatia ya tarehe 12 na 13.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269