Breaking News

Your Ad Spot

May 30, 2015

JAMBO LEO YAICHABANDA BODABODA FC 2-1 TAMASHA LA BODABODA UKONGA


 Wachezaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, wakifanya mazoezi ya kupasha mwili muda mfupi kabla ya kuvaana na timu ya Bodaboda FC ya Wilaya ya Ilala, wakati wa Tamasha la Bodaboda kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Katika mechi hiyo, Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.

 Kikosi cha timu ya Gazeti la Jambo Leo kilichopambana na Bodaboda FC

 Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (wa pili kulia), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, muda mfupi kabla ya timu hiyo kukipiga na timu ya Bodaboda FC ya Wilaya ya Ilala, wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam jana.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.



 Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Bodaboda FC , muda mfupi kabla ya timu hiyo kukipiga na timu ya Gazeti la Jambo Leo, wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam

 Silaa akitoa mawaidha kwa timu hizo kabla ya mechi kuanza





 Mchezaji wa timu ya Jambo Leo,  Frank Balile (kushoto) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya Bodaboda, Sharif Mohamed

 Mlinda mlango Maganga Benjamin wa timu ya Bodaboda Wilaya ya Ilala, akiudaka mpira katikati ya wachezaji wa timu ya Jambo Leo 'Wagumu Stars' Zahoro Mlanzi (kushoto) na Ali Salum wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa. Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.

 Moja ya kizazaa langoni mwa Bodaboda FC iliyosababishwa na washambuliaji wa Jambo Leo

 Mshambuliaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, Ali Salum (katikati) akifunga bao la kwanza dhidi ya Bodaboda FC,wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.

Slaa akiwasalimia wachezaji wa timu hizo mbili

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages