Breaking News

Your Ad Spot

Jun 2, 2015

LORI LA MAFUTA LAUA WATU 70 NIGERIA

Lori la mafuta lawaua watu 70 Nigeria
Karibu watu 70 wamefariki huko mashariki mwa Nigeria baada ya lori la kubeba mafuta kushika moto.
Police wanasema huenda kilichosababisha moto huo ni ajali.
Walioshuhudia wanasema dereva wa gari hilo alishindwa kulidhibiti ndiposa likakosa mwelekeo na kutoka barabarani na kuwagonga watu waliokuwa wakisubiri usafiri katika kituo kimoja cha mabasi.
Mmoja ya waliokuwa wakishughulika kuwanusuru waliojeruhiwa amesema magari mengine 12 nayo yalishika moto.
Mwandishi wa BBC aliyeko Nigeria anasema mikasa ya ajali zinazohusu magari ya kubeba mafuta hutokea mara kwa mara nchini humo.
Miaka mitatu iliyopita ajali mbaya sana ya moto wa mafuta iliwaua zaidi ya watu 100 huko Niger Delta katika mkasa uliochangiwa na watu kuchota mafuta yaliomwagika baada ya gari kubwa la mafuta kupata ajali

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages