Breaking News

Your Ad Spot

Jun 15, 2015

MAALIMU SEIF ; CCM IJIANDAE KISEIKOLOJIA KUKABIDHI Z, BAR

Wafuasi wa CUF wakinadi picha za mgombea Urais wa Chama hicho Visiwani, Seif Shariff Hamad katika mkutano wa hadhara wa kumtambulisha mgombea huyo uliofanyika kwenye Viwanja vya Tibilinzi- Chake chake Pemba jana. Picha na Said Khamis
Pemba/Dar. Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ameitaka CCM kujiandaa kisaikolojia kukabidhi madaraka kwa chama chake baada ya Oktoba, akisema katika chama chake hakutakuwa na neno “kushindwa”.
Maalim Seif, ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, aliwataka vijana popote walipo kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi ili kujitayarisha na ushindi aliouita mkubwa.
Alitoa kauli hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya Tibirinzi, Chake Chake Pemba na kuhudhuriwa na maelfu ya wafuasi wa chama hicho kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar.
“Hakuna kushindwa CUF, kwa hivyo mawazo yenu yawe na kushinda tu. Vijana, hakuna kukaa ukasema ushamaliza kupiga kura, unakwenda kwako unasubiri ushindi. Hakuna hilo mwaka huu, lazima mjitahidi kulinda ushindi wenu,” alisema Maalim Seif.
Katibu huyo wa CUF alisema wananchi wa Pemba walioko Arusha, Mwanza na sehemu nyingine warudi kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura na kuwataka kutoacha fursa hiyo ambayo ni haki yao ya kidemokrasia.
Akitilia mkazo suala hilo, aliyekuwa waziri wa SMZ, Mansoor Yussuf Himid alimtaka Maalim Seif baada ya kupiga kura yake kurudi nyumbani na kuwaachia vijana kumkabidhi ushindi wa chama hicho.
Mansoor ambaye ni mshauri wa Maalim Seif, alisema vijana wasitarajie kuletewa ushindi katika kisahani cha chai, washiriki kikamilifu katika kupatikana ushindi wa chama hicho.
Mansoor alisema hatima ya ushindi wa Zanzibar ipo mikononi mwa vijana, hivyo wanapaswa kuhakikisha ushindi wa Zanzibar unapatikana katika ya mikono yao.
Akihutubia mkutano huo, Mwanasiasa Hassan Nassor Moyo alisema kazi ya Maalim Seif na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume kuleta umoja wa kitaifa si jambo jipya kwa kuwa lilianzia kwa Mzee Karume ambaye alitunga sheria kuondosha ubaguzi na kuwaweka wananchi wote wa Zanzibar kuwa kitu kimoja.
Uchumi
Katika hotuba yake ya takriban saa moja iliyorushwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha Star TV, Maalim Seif alisema Maalim Seif alisisitiza nia yake ya kuifanya Zanzibar kuwa na mamlaka kamili ili iondokane na adhabu ambazo siyo stahiki kwake.
Seif alisema Wazanzibari wamekuwa wakiadhibiwa kutokana na ufisadi unaofanywa na baadhi ya viongozi wa Bara.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages