Breaking News

Your Ad Spot

Jun 1, 2015

NYALANDU KUCHUKUA FOMU YA URAIS JUNI SABA MJINI DODOMA

Waziri wa mali asili  na utalii Lazaro Nyarandu na waumini mbalimbali baada ya Ibada ya jumapili Jijini Arusha katika Kanisa la KKKT  Diyoyosis ya Mjini Kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi .
Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu akibadilishana mawazo na Kada wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA  James Olemilia baada ya ibada ya jumapili iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Diyosisi ya mjini kati Arusha ambapo Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutaja rasmi kuwa tarehe 6 mwezi ujao atachukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kuwania urais .

Mpiga picha  wa Chanell ten Arusha Aristrides Dotto na Elia Mbonea mwandishi wa gazeti la Mtanzania wakifanya mahojiano na  Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu mara baada ya ibada ya jumapili  katika Kanisa la KKKT  Diyoyosis ya Mjini kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi.
 **************
WAZIRI wa Mali Asili na Utalii, Lazoro Nyalandu ambaye alishatangaza nia ya kukiomba chama Chake cha Mapinduzi (CCM) kumteua kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, anataraji kuchukua fomu ya kutimiza adhma yake hiyo Juni 7 mwaka huu mjini Dodoma.


ametangaza rasmi kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo baada ya kutangaza nia yake miezi saba iliyopita mkoani Singida.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana, Nyalandu ambaye ni Mbunge wa Singida Magharibi, baada ya kushiriki ibada ya jumapili  katika kanisa la KKKT Usharika wa mjini Kati Arusha.

Nyalandu anaungana na makada wengine wa CCM kuingia katika kinyang’anyiro hicho ambapo anasema mpango na dhamira yake ya kuwania kuteuliwa na chama chake uko palepale huku akijinasibu kuwa dunia itaandika historia pale atakapo ibuka kidedea kwa kupeperusha bendera ya ccm katika kinyang’anyiro hicho.

 “Mpango na dhamira yangu ya kuomba ridhaa ya Chama change kuniteua kugombea urais mwaka huu upo palepale na dunia itaandika historia pale nitakapo ibuka kidedea na kuipeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa mwaka huu,” alisema Nyalandu.

Waziri Nyalandu atakungana na makada na Mawaziri wakongwe katika siasa za Tanzania katika kuwania nafasi hiyo ndani ya CCM kama akina Edward Lowassa, Steven Wasira, Bernard Membe, Samuel Sitta, na wengineo wengi ambao tayari wameshatangaza nia na dhamira yao ya kuutaka urais.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages