Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm.
Na Nicodemus Jonas, Dar es Salaam
BADO?
Licha ya kunasa saini ya winga, Deus Kaseke na straika Malimi Busungu,
bado Yanga wamesema hawajaridhika zaidi, hivyo wanataka kuongeza nguvu
kwenye wingi zote- kulia na kushoto.Katika kufanikisha hilo, Kocha Mkuu,
Hans van Der Pluijm, anatarajiwa kushuka Bongo ndani ya wiki hii ambapo
ataambatana na wachezaji wawili wanaomudu wingi ya kulia na kushoto.
Habari
kutoka Yanga zinasema kuwa lilikuwa pendekezo la kocha mwenyewe, lakini
taarifa nzuri kwa Wanayanga ni kwamba nyota hao ni kama mapacha-
wanajuana kwa kina, kwani wote wanatokea timu moja inayoshiriki ligi kuu
nchini Ghana.
Taarifa
hizo zimekwenda mbali na kufafanua kuwa mbali na Ghana, pia mitego
imetegwa katika nchi nyingine tano ambazo ni Rwanda, Benin, Sierra
Leone, Zimbambwe na Nigeria.Nafasi ambazo zinatolewa macho zaidi ni beki
wa kulia ambaye anategwa nchini Benin, huku nchi nyingine wakiangalia
zaidi kuimarisha safu ya ushambuliaji na kiungo wa kati.
“Tumeamua
kuangalia zaidi kuimarisha winga zetu, ukiangalia Coutinho hana
msaidizi kama ilivyo kwa Kaseke. Na wote atakuja nao kocha akitoka
kwenye mapumziko huko Ghana, sijawajua majina ila wanatoka timu moja,”
kilisema chanzo hicho.
Katibu wa
klabu hiyo, Dk Jonas Tiboroha, alilithibitishia Championi Jumatatu
mpango wa kusaka wachezaji wa kimataifa, lakini kikwazo ni Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) kuchelewa kutoa msimamo wao juu ya ombi la kutaka
idadi ya wachezaji wa kigeni kuongezeka kutoka watano hadi nane.
“Ni kweli
kuna wachezaji wa kigeni tunawafuatilia kwa karibu lakini kama
unavyojua tayari tumejaza nafasi za wageni, kwa sasa tunasubiri tamko la
TFF ili tuangalie cha kufanya zaidi, lakini kuhusu ujio wa kocha na
wachezaji hajaniambia,” alisema Dk Tiboroha.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269