Breaking News

Your Ad Spot

Jun 1, 2015

PLUIJM ASHUSHA MAWINGA WAWILI HATARI YANGA

Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm.
Na Nicodemus Jonas, Dar es Salaam
BADO? Licha ya kunasa saini ya winga, Deus Kaseke na straika Malimi Busungu, bado Yanga wamesema hawajaridhika zaidi, hivyo wanataka kuongeza nguvu kwenye wingi zote- kulia na kushoto.Katika kufanikisha hilo, Kocha Mkuu, Hans van Der Pluijm, anatarajiwa kushuka Bongo ndani ya wiki hii ambapo ataambatana na wachezaji wawili wanaomudu wingi ya kulia na kushoto.

Habari kutoka Yanga zinasema kuwa lilikuwa pendekezo la kocha mwenyewe, lakini taarifa nzuri kwa Wanayanga ni kwamba nyota hao ni kama mapacha- wanajuana kwa kina, kwani wote wanatokea timu moja inayoshiriki ligi kuu nchini Ghana.
Taarifa hizo zimekwenda mbali na kufafanua kuwa mbali na Ghana, pia mitego imetegwa katika nchi nyingine tano ambazo ni Rwanda, Benin, Sierra Leone, Zimbambwe na Nigeria.Nafasi ambazo zinatolewa macho zaidi ni beki wa kulia ambaye anategwa nchini Benin, huku nchi nyingine wakiangalia zaidi kuimarisha safu ya ushambuliaji na kiungo wa kati.
“Tumeamua kuangalia zaidi kuimarisha winga zetu, ukiangalia Coutinho hana msaidizi kama ilivyo kwa Kaseke. Na wote atakuja nao kocha akitoka kwenye mapumziko huko Ghana, sijawajua majina ila wanatoka timu moja,” kilisema chanzo hicho.
Katibu wa klabu hiyo, Dk Jonas Tiboroha, alilithibitishia Championi Jumatatu mpango wa kusaka wachezaji wa kimataifa, lakini kikwazo ni Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuchelewa kutoa msimamo wao juu ya ombi la kutaka idadi ya wachezaji wa kigeni kuongezeka kutoka watano hadi nane.
“Ni kweli kuna wachezaji wa kigeni tunawafuatilia kwa karibu lakini kama unavyojua tayari tumejaza nafasi za wageni, kwa sasa tunasubiri tamko la TFF ili tuangalie cha kufanya zaidi, lakini kuhusu ujio wa kocha na wachezaji hajaniambia,” alisema Dk Tiboroha.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages