Mchezaji
wa timu ya soka wa waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC),
Martin Peter (jezi ya kijani kulia) akipambana na mmoja wa wachezaji wa
timu ya makipa, Ivo Mapunda.
Kikosi cha Baobab.
Na Mwandishi wetu
TIMU
ya soka ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC) Ijumaa hii
itacheza mchezo maalum wa kirafiki dhidi ya timu ya wafanyakazi wa shule
ya sekondari ya Baobab ya Bagamoyo.
Mchezo
huo umepangwa kuanza saa 10.00 jioni kwenye uwanja wa shule ya
sekondari ya Baobab na tmgeni rasmi atakuwa mkurgugenzi wa shule hiyo,
Hlafan Swai.
Mbali ya Swai, viongozi wengine wa shule hiyo watahudhuria mechi hiyo maalum kwa ajili ya kuhamasisha michezo shuleni hapo.
Mwenyekiti
wa Taswa FC, Majuto Omary amesema kuwa awali walipanga kucheza mechi
mbili, ya wanaume (mpira wa miguu) na wanawake (netiboli), hata hivyo
wachezaji wa Taswa Queens hawakuweza kuanza mazoezi na hivyo kulazimika
kufuta mechi hiyo.
Majuto
alisema kuwa wamepokea maombi kutoka uongozi wa shule hiyo na hasa
baada ya kutoa mwanafunzi bora kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne,
Nyakaho Marungu. Alisema kuwa wamehamasika kupata mwaliko huo ambapo
mechi hiyo itakuwa kama sehemu ya sherehe ya kufunga shule.
Baadhi
ya wachezaji wa Taswa FC wakataokuwepo katika mechi hiyo ni Ali Mkogwe,
Wilbert Molandi, Salum Jaba, Deogratius “Super Deo” Maganga, Julius
Kihampa, Sweetbert Lukonge, Elius Kambili, Zahoro Mlanzi, Frank Balile,
Mwarami Seif, Saidi Seif, Jose, Martin Peter, Athuman Jabir, Muhidi
Sufiani na Jabir Johnson.
Baadhi
ya wachezaji wa timu ya wafanyakazi wa shule hiyo ni John Kanakamfumu,
Herry Morris (kocha wa timu ya wanafunzi), Renatus Kavishe, David
Ntungi, Hadji Juma, Madata Lubigisa, Athuman Tippo na wengineo.
“Huu
ni mchezo wa kudumisha ushirikiano wetu kwani sisi ni waandishi wa
habari za michezo na pia ni wazazi, hivyo tunaweza kuwapeleka watoto
wetu kusoma kaika shule hiyo bora, hivyo nawaomba wachezaji wote wafike
kwa wingi ili kuona mechi hiyo ya aina yake,” alisema Majuto.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269