Hapa ikionesha fomu baada ya kukabidhiwa.
Kada
wa CCM Jumaa Mhina 'Pijei' (katikati), akipokea fomu ya kuwania ubunge
Jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam, kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya
Kinondoni, Athuman Sheshe leo mchana. Anaye shuhudia kulia ni Kada wa
chama hicho anayewania ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia CCM,
Ramadhan Ndanga 'Potipoti'.
Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe (kushoto), akimpa maelezo ya kufuata baada ya kukabidhiwa fomu hizo.
Waandishi wa habari wakimuhoji nini atawafanyia wananchi wa Jimbo la Kawe iwapo atachaguliwa.
Na Mwandishi Wetu
MUWANIA
nafasi ya Ubunge Jimbo la Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumaa
Mhina 'Pijei' amesema akipata nafasi hiyo atashirikiana na wananchi wa
jimbo hilo katika kutatua changamoto zilizopo.
Hayo
aliyasema wakati akichukua fomu ya kugombea nafasi hiyo Dar es Salaam
leo mchana na utaja vipaumbele vyake vya maendeleo atakayofanya.
Alisema
mwaka 2010 aligombea lakini katika kura za maoni ya ccm hazikutosha,
mwaka huu anaamini zitatosha na kulikomboa jimbo lililo mikononi mwa
wapinzani.
Alisema
kipaumbele chake ni ajira kwa vijana, elimu, miundimbinu ya barabara na
umeme na kuwa mafanikio hayo yatakuja iwapo atashirikiana kwa karibu na
wananchi hivyo aliomba wananchi kuto muangusha wakati ukifika.
Alisema
tayari ametoa ajira kwa vijana kwa kuwapa bodaboda ambazo zimepunguza
tatizo la ajira na vitendo vya uhalifu katika jimbo hilo.
Mhina
alisema kipaumbele kingine atakacho kitoa ni kuhakikisha anatumia
uzoefu wake wa ujasiriamali kwa kuwajengea uwezo wanawake na vijana kwa
kuwapa elimu na kuwawezesha kupata mikopo yenye riba nafuu ili kuinua
mitaji yao.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269