Breaking News

Your Ad Spot

Jul 15, 2015

WAKILI ELIAS NAWERA ACHUKUA FOMU ZA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KAWE JIJINI DAR ES SALAAM

Wakili Elias Nawera akionyesha alama ya dole baada ya kukabidhiwa fomu hizo. Kulia ni mgombea ubunge mkoa wa Dar es Salaam kupitia Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Lilian Mkosani.
 Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe (kushoto), akimkabidhi fomu ya kugombea ubunge jimbo la Kawe, kada wa chama hicho, Wakili Elias Nawera (katikati), Dar es Salaam leo mchana. Kulia ni mgombea ubunge mkoa wa Dar es Salaam kupitia Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Lilian Mkosani
 Wakili Nawera (kulia), akiandika jambo kabla ya kulipa sh. 100,000  ya kuchukulia fomu.
 Hapa akimshukuru Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe baada ya kuchukua fomu hizo.
 Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe (kushoto), akimuelekeza Wakili Elias Nawera mambo ambayo anapaswa kuyafuata baada ya kukabidhiwa fomu hizo.
Mbunge wa Jimbo la Kinondoni ambaye anamaliza muda wake Iddi Azani akimpongeza Wakili Nawera baada ya kuchukua fomu hizo. Azan alifika katika ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni kwa ajili ya kuchukua fomu ya kutetea nafasi yake ya ubunge katika Jimbo hilo. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages