Mkurugenzi
wa Taasisi ya kinamama wa Kiafika inayohusika na ugonjwa wa Saratani ya
matiti Bi. Ify Nwabuku(kushoto) akizungumza na wakina mama (hawapo
picha) wakati wa utoaji wa matibabu bure kwa wakina mama katika
hospitali ya Mwananyamala jijini Dar. Kushoto ni Bi Asha Nyang'anyi
ambaye ni mwanakamati wa ustawi wa jamii na maendeleo ya kiuchumiwa
jumuiya ya Watanzania DMV.
Wakina
mama wakimsikiliza kwa makini Bi. Ify Nwabuku wakati akitoa maelezo juu
ya upimaji wa Saratani kwa wakina mama waliofika kupima afya zao katika
hospitali ya Mwananyamala zilizokuwa zikitolewa na Jumuiya ya
Watanzania DMV pamoja na washirika wao walioamua kutoa huduma za
kitabibu na madawa bure.
Dk.
George Quintero(kushoto) kutoka Marekani akimtibu meno mtoto Living
Andrew aliyeshikwa na mama yake huku akisaidiana na Dk. Emilton
Ndashau(kulia) wakatia wa utoaji wa uduma bure iliyodhaminiwa na Jumuiya
ya Watanzania DMV pamoja na washirika wao katika Hospitali ya
Mwananyamala jijini Dar.
Dk.
Somtochukwa Agunwah(kushoto) kutoka Marekani akimtibu mmoja wa mama
aliyekuwa anaumwa jino katika hospitali ya Mwananyamala huku akisaidiwa
na Dk. Kilechi Nwankwo(kilia) kutoka Marekani pamoja na Dk. Kisumo
Armogaston.
Dk.
William Desdery ambaye ni daktari wa macho akimtibu mmoja wa wakina
mama waliofika katika hospitali ya Mwananyamala jijini dar kwa ajili ya
matibabu yanayotolewa bure na Jumuiya ya Watanzania DMV pamoja na
washirika wao.
Dk.
Sharon Sagoo akipima dawa zilizotolewa na Jumuiya ya Watanzania DMV
pamoja na washirika wao kwa ajili ya kupewa mgojwa waliokuwa wanaumwa
katika hospitali ya Mwananyamala
Dk. Jummy Amuwo akihakiki madawa
Hizi
ni baadhi ya Dawa zilizotolewa na Jumuiya ya Watanzania DMV pamoja na
washirika wao kwa ajili ya wagonjwa wa Hospitali ya Mwananyamala na pia
zinatolewa bure.
Rais
wa Jumuiya ya Jumuiya ya Watanzania DMV, Bw. Iddi Sandaly(kustoto)
akiwa kwenye picha ya pamoja na Bi. Adama Gibateh(katikati) pamoja na
Kushoto ni Bi Asha Nyang'anyi ambaye ni mwanakamatiwa ustawi wa jamii na
maendeleo ya kiuchumiwa jumuiya ya Watanzania DMV.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269