Breaking News

Your Ad Spot

Sep 29, 2015

USIKU WA ESTER DIANA NANA, ALIVYOMEREMETA

 Bi Harusi mtarajiwa Ester Diana Nana (kushoto) akigonisha glasi na msimamizi wake, Hellen, wakati wa sherehe ya kuagwa (Send off) iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.

 Ester akikata keki huku akisaidiana namsaidizi wake

 Bi Harusi mtarajiwa Ester Diana Nana (kushoto) akimlisha keki msimamizi wake, Hellen, wakati wa sherehe ya kuagwa (Send off) iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.

 Bi Harusi mtarajiwa Ester Diana Nana akimkabidhi keki, Naibu Katibu Mkuu wa Ofoso ya Makamu wa Rais, Bi. Angelina Madete, wakati wa sherehe ya kuagwa (Send off) iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.(P.T)

 Mwendesha Shughuli Mc Bazil, akifanya yake katika sherehe hiyo
 Mama Mzazi wa Bi harusi mtarajiwa, akimkabidhi zawadi ya Biblia mwanae Ester
 Wakwe wakiandaa zawadi ya Bi harusi mtarajiwa kabla ya kumkabidhi
 Mc Bazil. akimkabidhi zawadi ya Cd Bi Harusi mtarajiwa ukumbini hapo
 Wakati wa zawadi.....
Bi harusi mtarajiwa akiwa na mumewe mtarajiwa wakielekea kupata chakula cha usiku ukumbini hapo. Watarajiwa hao wanatarajia kufunga ndoa jumamosi ya wiki hii.
Wakati wa mlo wa usiku

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages