Watu watatu sasa
wamethibitishwa kufariki baada ya daraja la mda kuangukia barabara kuu
ya magari mjini Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya jumatano.
Watu wengine 19 walijeruhiwa katika kisa hicho ,kulingana na shirika la huduma za dharura nchini humo.
Meya
wa Johannesburg amesema kuwa iwapo uchunguzi wao utabaini kwamba
kuanguka kwa daraja hilo kunatokana na uzembe, wale waliohusika
watawajibishwa kulingana na mwandishi wa BBC Pumza Filhani mjini humo.
Kampuni ya ujenzi nchini Afrika Kusini Murray & Robert imeanzisha uchunguzi wake.

No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269