Breaking News

Your Ad Spot

Oct 30, 2015

RAIS MTEULE WA TANZANIA, DK. JOHN MAGUFULI AKABIDHIWA CHETI CHAKE CHA USHINDI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais Mteule wa awamu ya tano, Dk. John Magufuli akiyonyesha hati ya ushindi wa Urais, baada ya kukabidhiwa leo na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva, katika hafla ya kukabidhi hati hiyo iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Dk. Magufuli amekabidhiwa cheti hicho kufuatia kuibuka mshindi wa kiti cha Urais katika matokeo yaliyotangazwa na NEC, jana, ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu. Kushoto ni Makamu wa Rais Mteule, Mama Samia Suluhu Hassan.
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva akimkabidhi hati ya Ushindi Makamu wa Rais Mteule, Mama Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Dk. John Magufuli
  Mama Samia akionyesha hati baada ya kukabidhiwa
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu, Damian Lubuva akiwapongeza Rais Mteule Dk. Magufuli, na Makamu wake Mteule,
Rais Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli akipongezana na Makamu wake pia Mteule, Mama Samia Suluhu Hassan, baada ya kukabidhiwa hati zao za ushini na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Msaafu Damaian Lubuva, leo Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
 Rais Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli akimuonyesha hati ya ushindi, aliyekuwa Mgombea Urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Anna Mghwira, baada ya kukabidhiwa hati hiyo na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
 Rais Jakaya Kikwete akimpongeza Rais Mteule, Dk. John Magufuli, baada ya kukabidhiwa hati ya ushindi wa kiti cha Urais
 Dk. Magufuli akimpa akishike cheti hicho Rais Jakaya Kikwete
 'Sasa ni huyu" Rais Kikwete akichombeza wakati alipoonyeshwa cheti cha ushindi wa Urais na Dk. Magufuli
 Rais Mteule Dk. Magufuli akimpongezwa na Mkewe Mama Jannet Magufuli, baada ya kukabidhiwa hati ya ushindi wa Urais. Kushoto ni mke wa Rais Mama Salma Kikwete. na kulia ni Makamu wa Rais Mteule  Mama Samia Suluhu Hassan
 Dk. Magufuli akipongezwa na Dk. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Katikati yao ni Rais Jakaya Kikwete na Kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda
 Mama Samia akipongezwa na Mama Salma Kikwete. Kushoto ni Rais Kikwete
  Dk. Magufuli akipongzwa na Makamu Mwenyekiti mstaafu, wa CCM, Pius Msekwa. Katikati yao ni Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi
 Rais Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli akipongezwa na Rais Mstaafu wa Nigeria Goodluck Jonathan, baada ya kukabidhiwa hati
 Dk. Magufuli akionyesha hati yake kwa wananchi baada ya kukabidhiwa hati hiyo
 Wadau wakiwa ukimbini
 Makamu wa Rais Mteule, Mama Samia akiwapungia wananchi mkono baada ya kupewa hati yake
 Mama samaia akiwasalimia wananchi ukumbini baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi
 Aliyekuwa Mgombea Urais kwa tiketi ya ACT, Anna Mghwira akimpongeza Dk. Magufuli, kwa ushindi aliopata
Picha ya pamoja
 Picha ya pamoja
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akimpongeza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubuva  baada ya kukabidhi cheti cha Usnhindi wa Urais kwa Dk. Magufuli. Wapili ni Rais Kikwete na kulia ni Mama Samia
 Picha ya pamoja, Dk. Magufuli, Rais Kikwete, Mama samia na Jaji Mstaafu Lubuva
 Picha ya pamoja
 Rais wa Zamani wa Naigeria Goodluck Jonathan akiwa katika picha ya pamoja na Dk. Magufuli,  Rais Jakaya Kikwete, Mama Samia na Spika wa Bunge Anna Makinda
 Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi akimpongeza Dk. Magufuli
 Picha ya Pamoja, Dk. Magufuli na Viongozi wa dini waliohudhuria
 Mwenyekiti wa IPP Reginarl Mengi naye alikuwepo. Hapa anateta jambo na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyage


 Wabungewateule, Dk. Faustine  Ndungulile wa Kigamboni na Nape Nnauye wa Mtama wakipongezana baada ya kukutana kwenye hafla hiyo
 Nape akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kwenye hafla hiyo
 Wajumbe wa iliyokuwa Kamati ya Kampeni za CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi, Abdallah Bulembo na Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mama Zakiah Meghji wakisalimiana kwa bashasha na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambaye ni Mbunge Mteule wa Mtama wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakati wa hafala hiyo
Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi akimsikiliza kwa makini Katibu wa NEC, Itikadi na uenezi Nape Nnauye wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya viongozi wa CCM, wakiwa kwenye hafla hiyo
Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula akisalimia baadhi ya viongozi baada ya kuwasili kwenye hafla hiyo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akizungumza jambo na Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue wakati wa hafla hiyo
Baadhi ya viongozi mashuhuri wakiwa kwenye hafla hiyo
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jai Mstaafu Sinde Warioba, akiwa na Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, John Malecela wakati wa hafla hiyo
Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Pius Msekwa akizungumza na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakati wa hafla hiyo. Wengine ni Spika wa Bunge anne Makinda na Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Hali ya meza kuu ya Viongozi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na waliokuwa wagombea wa Urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 2015, ilivyokuwa kabla ya shughuli kuanza
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishauriana jambo na mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete meza kuu.
Rais Mteule, Dk. John Magufuli akiondoka kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee baada ya kukabidhiwa cheti chake cha kushinda Urais
Mama akiwa na mtoto wake wote wakiwa wamevalia nguo za CCM, wakati wa mapokezi ya Rais Mteule Dk. John Magufuli kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza kumkaribisha Rais Mteule, Dk. John Magufuli kuzungumza na hadhara kwenye sherehe fupi ya mapokezi iliyofanyika leo kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam
Rais Mteule Dk. John Magufuli akizungumza na wananchi katika mapokezi yaliyofanyika leo kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam
Wananchi waliompokea Rais Mteule Dk. John Maguli wakishangilia wakati wa mapokezi hayo Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam
Wananchi waliompokea Rais Mteule Dk. John Maguli wakishangilia wakati wa mapokezi hayo Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam
Rais Mteule Dk. John Magufuli akiwahutubia wananchi hao
Makamu wa Rais Mteule, Mama Samia Suluhu Hassan, akionyesha cheti chake cha ushindi
Dk. John Magufui akizungumza na wananchi huku akiwa na Makamu wake wa Rais Mteule Mama Samia
Rais Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli akimtambulisha mkewe, Mama Janneth Magufuli wakati wa hafla hiyo.
Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais Mteule Dk. John Magufulu wakati wa hafla hiyo
Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais Mteule Dk. John Magufulu wakati wa hafla hiyo ya mapokezi iliyofanyika leo kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages