Breaking News

Your Ad Spot

Oct 25, 2015

TASWIRA MBALI MBALI KATIKA MKUTANO WA KUFUNGA KAMPENI ZA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA TEMEKE, ABBAS MTEMVU JIJINI DAR

 Mgombea Ubunge Abbas Mtemvu akizungumza na Wanancha na Wanachama wa CCM akisisitiza jambo wakati wa kufunga Kampeni katika Kata ya Kilakala Dar es Salaam jana. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
 Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu akiwa anacheza pamoja na wanachama wakati alipokuwa akienda jukwaani kuhutubia Mkutano wa Lala salama wa Kampeni kabla ya kufungwa mkutano huo uliofanyika katika Kata ya Kilakala Dar es Salaam
 Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu akihutubia wananchi na wanachama wa Kilakala katika Mkutano wa Kampeni za lalasalama na kuwaomba wajitokeze kwa wingi mapema kutimiza haki yao ya msingi kwa kupiga kura na kuondoka kurudi majumbani
 Wananchi na wanachama wakisikiliza kwa makini Mgombea Ubunge Abbas Mtemvu alipokuwa akihutubia Mkutano wa Kampeni kabla ya kufungwa mkutano huo Dars es Salaam


 Mgombea Udiwani Kata ya Kilakala Amiri Osama akihutubia Mkutano huo kabla ya kufungwa mkutano huo wa Lalasalama uliofanyika katika Kata ya Kilakala

 Mgombea Ubunge Abbas Mtemvu (wa tatu kushoto) akipiga makofi walipokuwa wakiimba wimbo baada ya Katibu CCM Mkoa wa  Dar es Salaam Abdallah Mihewa (wakwanza kushoto) kufunga Mkutano wa Kampeni uliyofanyika Kata ya Kilakalala Dar es Salaam

 Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke CCM, Abbas Mtemvu (wakwanza kushoto) akisaini katika kitabu cha wageni  alipotembelea Ofisi za Keko Mwanga 'B' alipokuwa akizindua Mashina ya wakereketwa wa Chama hicho ambapo jumla ya mashina 11 yamezinduliwa na kuhudhuria Mikutano 3  na kuvuna wanachama wapya 16 akiwemo Mmoja toka chama cha Upinzani, kulia ni Mwenyekiti wa chama hicho Frank Otaigo
 Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu akiongea na Wanachama wa Shina la wakereketwa la Akinamama Jeshi Kubwa


 Msafara wa Mgombea Ubunge


 Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu (aliyevaa kofia kulia) akimsikiliza mlezi wa Caw Wosh Taifa Fortunatus John (watatu kushoto) wakati Mgombea huyo  alipofika katika Shina hilo kuzindua Shina hilo

 Wananchi wakipungia mikono msafara wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu ulipokuwa ukipita eneo la kurasini

 Mama Mtemvu akisalimiana na  wananchi na wanachama wa Chama hicho


  Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu akisalimiana na wananchi wa Kurasini

 Wananchi wakiwa na furaha ya kuona mgombea Ubunge akipita na msafara alipokuwa akienda katika Mkutano wa Lalasalama uliofanyika kurasini Shimo la Udongo Dar es Salaam

  Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu akiwa anaingia kwenye Mkutano wa Lalasala  eneo la Kurasini

  Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu na Mkewe Mama Mtemvu wakiingia katika Mkutano wa Lalasalama huku wakiwapungia Mikono Wananchi na Wanachama 
 Mwanafunzi wa Darasa la Pili wa Shule ya Msingi Minazini Iliyopo Kurasini,  Mwanahamisi Ally akiwa ameshika bango lenye nembo ya picha ya  mgombea Urais kupitia CCM
 Mwanafunzi wa Darasa la Pili wa Shule ya Msingi Minazini Iliyopo Kurasini,  Mwanahamisi Ally (kushoto) aliyekaakwenyekiti akiwa ameshika bango lenye nembo ya picha ya  mgombea Urais kupitia CCM, akiwa na magongo yake akiuguza mguu wake wa kulia uliokuwa umefungwa POP  baada ya kugongwa na Pikipiki
 Wasanii wa kundi la The Hirouse kurasini wakitowa burudani katika Mkutano wa Kampeni za Lalasalama uliofanyika Kurasini Shimo la Udongo Dar es Salaam jana
 Mwanafunzi chipukizi anayesoma Darasa la 5 katika  shule ya Msingi Kurasini Ally Juma (11) alipokuwa akiwasalim wana Chama cha Mapinduzi  katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika Kurasini Shimo la Udongo Dar es Salaam 
 Mwanafunzi chipukizi anayesoma Darasa la 5 katika  shule ya Msingi Kurasini Ally Juma (11) alipokuwa akiwaombea kura wagombea wa Chama cha Mapinduzi kuanzia kwa ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika Kurasini Shimo la Udongo Dar es Salaam







 Mama Mtemvu akiwa jukwaani akiwasalim na kuwaombea kura Wagombea wote wa CCM kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge na  Udiwani










 Mratibu wa Kampeni Jimbo la Temeke na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (W) Temeke Mustafa Hakika,  akimnadi Mgombea Udiwani kupitia CCM, Wilfred Kimati wa Kurasini
 Mratibu wa Kampeni Jimbo la Temeke na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (W) Temeke Mustafa Hakika (kushoto),  akimnadi Mgombea Ubunge kupitia Chama hicho, Abbas Mtemvu wakati wa Mkutano wa Lalasama  uliyofanyika Kurasini Shimo la Udongo  Dar es Salaam jana


 Mgombea Ubunge Abbas Mtemvu akimvisha kofia Mmoja wa wanachama waliojiunga na Chama hicho kwenye Mkutano wa Kampeni uliofanyika Kurasini Shimo la Mchanga
 Wanacha wapya 16 kuingia CCM wakila kiapo baada ya kuingia chama hicho

 Wananchi wakiupungia msafara wa Mgombea Ubunge















No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages