Breaking News

Your Ad Spot

Dec 23, 2015

TPB YATOA ZAIDI YA MILIONI 200 KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI KIUCHUMI, NI MKOPO NAFUU

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania, TPB, Sabasaba Moshingi, (kushoto), akikabidhi mfano wa hundi kwa Mkurugenzi wa Shirika la Vijana Wajasiriamali na Uwezeshaji Tanzania, (TYEEO), Ayub Gerald Luhuga, wakati wa hafla fupi iliyofanyika Wizara ya Fedha na Mipango, jijini Dar es Salaam Desemba 23, 2015.
        Benki hiyo imevipatia vikundi vinane vya wajasiriamali jumla ya shilingi 244,500,000/- kama mpoko nafuu ikiwa ni awamu ya kwanza ya utoaji mikopo hiyo, kufuatia makubaliano baina ya benki hiyo na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC), kudhamini vikundi hivyo ili vifungue akaunti TPB na kujipatia mikopo huku NEEC ikiwa ndio wadhamini wakuu. Jumla ya shilingi bilioni 2 zimetengwa kwa lengo hilo. Wanoshuhudia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa NEEC, Anna Dominic, (wapili kushoto) na afisa wa baraza hilo
  Bw. Moshingi akisalimiana na wana VICOBA

NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
BENKI ya Posta Tanzania, TPB, imekabidhimkopo wa  jumla ya shilingi 244,500,000/- kwa vikundi vinane vya wajasiriamali.
Makabidhiano hayo yamefanyika leo Desemba 23, 2015 kwenye hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC).
Akizungumza kwenye makabidhiano hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, fedha hizo ni awamu ya kwanza ya benki kutoa mikopo hiyo yenye masharti nafuu, baada ya kutiliana saini na NEEC Julai mwaka huu wa 2015, ambapo baraza hilo litadhamini vikundi hivyo ambavyo vitapaswa kwanza kufungua akaunti TPB kabla ya kupatiwa mikopo hiyo ambayo jumla ya shilingi bilioni 2 zimetengwa kwa dhumuni hilo.
“Ninayo furaha kubwa kuwakabidhi nyinyi wajasiriamali ili muweze kutimiza ndoto zenu za kujikwamua kiuchumi.” Alisema Bw. Moshingi na kuhimiza vikundi zaidi vya  wajasiriamali kujiunga na benki hiyo ili navyo vifaidi kwa wanachama wake kujiongezea mitaji kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, mgeni rasmi ambaye ni Kaimu Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi. Anna Dominic, alisema, baada ya NEEC kuona takwimu zinaonyesha kuwa hapa nchini ukosefu wa ajira ni moja ya changamoto kubwa kabisa na hivyo inahimiza wananchi kujiunga kwenye vikundi ili NEEC kwa kushirikiana na taasisi nyingine kama TPB, kuweza kuwapatia mikopo kwa ajili ya kufanya shughuli za kiuchumi.
“Ningependa kuwaasa wajasiriamali mliopokea mikopo hiyo, kufanya kazi kwa bidii kama ulivyo msimamo wa serikali ya awamu ya tano chini ya Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya “Hapa Kazi Tu”.” Alisema na kuwahimiza kutumia vizuri mikopo hiyo kwa shughuli zilizokusudiwa ili waweze kurejesha tena kwa wakati.
Akitoa shukrani zake baada ya kupokea mkopo huo kwa niaba ya wenzake, Mkurugenzi wa Shirika la Vijana Wajasiriamali na Uwezeshaji Tanzania, (TYEEO), Bw. Ayub Gerald Luhuga, aliishukuru TPB kwa kuwaunga mkono katika kuhakikisha wajasiriamali wanakuza mitaji yao ili kujikwamua kiuchumi, na kuahidi kuwa mikopo hiyo itatumika kama ilivyokusudiwa na kurejeshwa kwa wakati.


  Bi. Anna akitoa hotuba yake

 Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo ya TPB, Bw.Henry Bwogi, (kulia), Mkurugenzi wa Masoko wa TPB, Bw.Deogratius Kwiyukwa, (katikati), na Meneja Mikopo ya Vikundi ya TPB, Bw.Ramadhan Liganga, wakibadilishana mawazo



 Bw.Moshingi, (kushoto), akimsikiliza Bw. Kwiyukwa, huku Afisa Habari Mwandamizi wa TPB, Bw.Theo Mwakifulefula akisikilzia Mmoja wa wajasiriamali akipiga makofi kufurahia jambo






 Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo ya TPB, Bw.Henry Bwogi,(kushoto) na Mkurugenzi wa Masoko wa TPB, Bw.Deogratius Kwiyukwa, (katikati), wakimsikiliza mkurugenzi wa TYEEO, Bw. Ayubu

 Bw. Ayubu akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wajasiriamali wenzake
 Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages