Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai) akiwasalimia
wananchi wanaosubiri kupata huduma ya Hati za Kusafiria katika Ofisi za Makao
Makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam leo Desemba 23, 2015. Waziri Kitwanga alifanya
ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la kujifunza kazi mbalimbali
zinazofanywa na Uhamiaji. Katika hotuba yake, licha ya maelekezo mengine aliyoyatoa
kwa viongozi wakuu, pia aliitaka Idara hiyo ya Uhamiaji kuanza rasmi kwa operesheni
ya kuwasaka na kuwakamata wahamiaji haramu popote walipo nchini na kuagiza msako huo kuanza mara moja Januari 1, 2016. (Picha
zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile
(kushoto) akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, wakati
Waziri huyo alipokuwa anafanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji,
Kurasini, jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali
zinazofanywa na Uhamiaji
Afisa
Uhamiaji anayeshughulika na uchapaji wa Hati za
Kusafiria, Amir Hassan (kushoto),
akitoa maelezo ya jinsi wanavyozichapisha Hati za Kusafiria, kwa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) ambaye alifanya ziara ya
kikazi katika ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam.
Kulia ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,
Sylvester Ambokile
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile
akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga
(katikati) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji,
Kurasini, jijini Dar es Salaam leo
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiwaeleza jambo
Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao
Makuu ya idara hiyo, Kurasini, jijini Dar es Salaam leo. Wapili kushoto ni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil, na kushoto
ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo, na wapili kulia (waliokaa) ni
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester
Ambokile na kulia ni Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha), Piniel Mgonja
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles
Kitwanga (wasita kulia), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (watano
kushoto), Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo (wanne kushoto) wakiwa katika picha ya
pamoja na Viongozi Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati Waziri huyo alipotembelea
Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Wasita kushoto ni Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji, Sylvester Ambokile
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akimsalimia Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile wakati alipowasili Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil, na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Katika ziara hiyo, Waziri Kitwanga aliitaka Idara hiyo ya Uhamiaji kuanz rasmi kwa operesheni ya kuwakamata Wahamiaji Haramu nchini
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269