Breaking News

Your Ad Spot

Jan 27, 2016

JAJI MASHUHURI ANASWA KWA RUSHWA, KAMATI HUDUMA ZA KIMAHAKAMA KUMJADILI LEO JUMATANO



·         NA K-VIS MEDIA Na Mashirika ya Habari
·          
·         JAJI wa Mahakama Kuu nchini Kenya Philip Tunoi(Pichani), mwenye umri wa miaka 72 anatuhumiwa kula “kula_ mlungula kiasi cha shilingi za Kenya Milioni 2.
·          
·         Jaji huyo ambaye anatarajiwa kufikishwa mbele ya Tume ya Huduma za Mahakama (Judiciary Service Commission-JSC), Jumatano Januari 27, 2016, amewatuhumu baadhi ya majaji wenzake kuwa ndio walioanzisha “figisufigisu” ili yeye aondolewe na wachukue nafasi yake. Gazeti la Standard la Kenya limeripoti leo
Jaji huyo ameendelea kujitetea kuwa kundi hilo la majaji na baadhi ya mawakili, wamefikia hadi kuomba afe kwa vile tu alikataa kustaafu wakati akiwa na umri wa miaka 70.
Tuhuma zenyewe ni kwamba, jaji huyo mashuhuri nchini Kenya, alipokea rushwa ya shilini milioni 200 kutoka kwa Gavana wa Nairobi Evans Kidero ili kupindisha matokeo ya pingamizi mbunge wa Kabete, Ferrdinand Waititu akipinga kuchaguliwa kwa Gavana huyo na kutuhumu kuwa Gavana huyo alimtumia mu mmoja aitwaye Geofrey Kiplagat.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, limemnukuu Bw. Kiplagat akisema kuwa sekeseke hilo la rushwa lilianza mwezi Mei, 2014 ambapo aliombwa na mfanyabiashara mmoja kupitia njia ya simu kama ataweza kumuunganisha na Jaji Tunoi kumsaidia kwenye kesi dhidi ya Dkt. Kidero.
Kiplagat ameliambia gazeti hilo kuwa baada ya kukamilisha mipango hiyo na kwenda sawa,Jaji huyo alikabidhiwa mlungula huo (rushwa),  kwenye kituo kimoja cha mafuta jijini Nairobi.
Kufuatia tuhuma hizo, gazeti hilo limeripoti leo kuwa Jaji Mkuu  wa Kenya, Dkt. Willy Mutunga, ametangaza kikao maalum cha kamati ya huduma za kimahakama  itakaa kushughulikia suala hilo ambalo limeichafua Mahakama Kuu ya Kenya.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages