Baadhi ya madiwani wakifuatilia mkutano huo. |
Baraza la Madiwani likiendelea na vikao. |
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
BAJETI ya Manispaa ya Ilala kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ni sh.bilioni 55 kutoka sh.bilioni 30 ya mwaka wa fedha 2014/2016.
Akizungumza
katika baraza la madiwani katibu wa baraza hilo na Mkurgenzi wa
Manispaa ya Ilala, Isaya Mngurumi amesema kuwa kutokana na bajeti hiyo
kuwa juu madiwani wanatakiwa kufanya kazi katika kubuni vyanzo vya
mapato.
Amesema
kuwa baraza ndilo linaweza kufanya bajeti hiyo ikatimia katika
makusanyo kutokana na vyanzo vya mapato vilivyopo au kuongeza vyanzo
vingine.
Mngurumi
amesema katika kuanza kufanya kazi kwa baraza la madiwani lazima kamati
zipatikane ambapo hilo limefanyika kwa kufanya uchaguzi.
Aidha
amesema kuendana na bajeti hizo kamati ziweze kujadili bajeti jinsi ya
kuweza kupata bajeti itakayosaidia kuendesha na kutoa huduma kwa
wananchi wa manispaa ya Ilala.
Meya wa Manispa kwa ya Ilala, Charles Kuyeko amewataka madiwani kujadili kwa kina bajeti hiyo katika kamati.
01.Mkurgenzi
wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mngurumi akizungumza na baraza la madiwani
juu ya bajeti kuwa juu madiwani wanatakiwa kufanya kazi katika kubuni
vyanzo vya mapato,leo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269