Breaking News

Your Ad Spot

Feb 17, 2016

BENNETT : MAREKANI IMELIPA KUNDI LA DAESH SILAHA ZA KEMIKALI

Bennett: Marekani imelipa kundi la Daesh silaha za kemikali
Afisa wa zamani wa jeshi la Marekani amesema kuwa silaha za kemikali zinazomilikiwa na kundi la Daesh zimetoka Marekani.
Katika mahojiano yake ya IRIB, Scott Bennett ambaye aliwahji kuwa afisa wa jeshi la Marekani amelaani jinai zinazoendelea kufanywa na wapiganaji wa kundi la kigaidi la Daesh katika nchi za Iraq na Syria na kusema, kundi hilo linamiliki silaha za kemikali kutoka Marekani na kwamba lilipata silaha hizo hatari kupitia Saudi Arabia na Uturuki.
Bennett amesema kuwa Serikali na Congresi ya Marekani zimelipa kundi hilo la kigaidi silaha hizo za kemikali kwa makusudi ili litimize malengo ya Washington katika eneo la Mashariki ya Kati. Afisa huyo wa zamani wa jeshi la Marekani ameongeza kuwa, Washington imeshindwa kufikia malengo yake nchini Syria kwani licha ya miaka kadhaa ya ngogoro wa ndani nchini humo Wasyria bado wana imani na serikali ya Rais Bashar Assad na wanashiriki katika medani za vita dhidi ya kundi la Daesh kwa lengo la kurejesha amani na utulivu katika nchi yao.
Mgogoro wa ndani wa Syria ulianza mwaka 2011 kufuatia hujuma na mashambulizi makubwa ya makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na Marekani na waitifaki wake wakubwa kama Saudi Arabia kwa shabaha ya kuiondoa madarakani serikali halali ya Rais Bashar Assad.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages