Breaking News

Your Ad Spot

Feb 3, 2016

KAMPUNI YA SIMU YA TIGO YAANZISHA HUDUMA YA WHATSAPP BURE KWA WATEJA WAKE

 Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez akizungumza na waandishi wa habari na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika Hoteli ya Hyatt Regence Kilimanjaro Dar es Salaam jana.
 Wadau mbalimbali na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Hapa kila mgeni mualikwa akiwa busy na simu yake kwenye uzinduzi huo.
 Ni kama wanasema 'tumependeza sana ngoja tujipige picha'.
 Wanahabari wakifurahia jambo kwenye uzinduzi huo.
 Hapa ni furaha tupu kwa wanahabari.
 Washereheshaji katika uzinduzi huo, Taji Lihundi na mwenzake wakifanya vitu vyao.
 Burudani ikiendelea.
 Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez  (katikati), akiwa na viongozi wenzake katika uzinduzi huo.
  Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez  (katikati), akiwa na washereheshaji wa uzinduzi huo.
 Makofi yakipigwa kufurahia uzinduzi huo.
Wanahabari mabloggers wakiwa katika picha ya pamoja na msanii Lucas Muhuvile 'Joti'.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya simu ya mkononi ya Tigo, imetangaza huduma ya bure ya WhatsAap kwa watumiaji wa huduma hiyo.

Akizungumza Dar es Salaam jana katika uzinduzi huo,Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez amesema kuwa wateja waote wa tigo wanaotumia vifurushi vya intaneti vya kampuni hiyo kwa wiki na mwezi watapata huduma ya whatsaap bure.

Alisema kuwa  ni mara ya kwanza kwa kampuni ya simu kitoa ofa ya bure ya mtandao huo wa jamii nchini pia kampuni ya tigo ina wateja zaidi ya milioni 10.

"Unajua huduma ya whatsaap ambayo ni maarufu kwenye kutumia ujumbe kwa njia ya simu inawatumiaji zaidi ya milioni nane nchini tanzania na duniani inatumiwa na watu wapatao milioni 900,pia huduma hiyo inasaidia watumiaji kubadilishana habari ,ujumbe,video na miito ya sauti"alisema Gutierrez

Alisema kuwa kuanzia sasa na kuendelea kwa wateja wote wa tigo wanaonunua vifurushi vyetu vya wiki au mwezi watakuwa na fursa ya kufurahia whatsaap bure.

Aliongeza kuwa huduma ni kwa watumiaji wa smartphone na kupata huduma bure ya whatsaap kwa wateja tigo imejikita katika kuboresha mabadiliko kwenye maisha ya kidigitali.


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages