Mkurugenzi wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa
Mataifa (UNDCF), David Jackson, (kulia), akiwa kwennye mahojiano na Mjumbe
kutoka nchini Uganda, Naibu Mkurugenzi wa usimamizi wa mikakati na maendeleo ya
biashara wa jiji la Kampala, Patrick Musoke, pembezoni mwa mkutano wa siku mbili
wa wataalamu wa fedha na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali
Duniani, kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam,
Februari 29, 2016. (Picha zote na K-VIS MEDIA/Khalfan Said)
Washiriki wa mkutano wa kimataifa wa siku mbili
wa wataalamu wa masuala ya fedha na wadau wa maendeleo wakifuatilia mada
ikliyorushwa kwa njia ya video na Profesa Paul Smoke kutoka Chuo Kikuu Cha New
York, nchini Marekani.
Mshauri wa masuala ya fedha, Jesper Steffensen,
akitoa mada kwenye mkutano huo
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa
Mataifa (UNDCF), David Jackson, (kulia), akizungumza kwenye mkutano wa siku
mbili wa wataalamu wa fedha na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali
Duniani, kwenye hoteli ya Hyaatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam,
Februari 29, 2016. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Serikali za Mitaa
nchini Uganda, John Genda Walala
Na
Mwandishi wetu
WATAALAMU wa fedha na wadau wa
maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali duniani wameanza mkutano wa siku mbili jijini Dare s Salaam kuangalia namna
ya kuwezesha fedha za kusaidia maendeleo endelevu kwenye manispaa na majiji kwa kutumia
vyanzo vya ndani.
Mkutano huo wa siku mbili ulioanza leo Februari 29, 2016 katika
hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro umelenga kuja na maelezo muafaka ya namna
ya kupata fedha za kuendesha na kujenga miundombinu mbalimbali kwa ajili ya
miji inayotanuka kwa kasi hivi sasa barani Afrika.
Katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi
kuhusu mkutano huo , Mmoja wa wakurugenzi wa UNCDF kutoka makao makuu
anayeshughulikia uendelezi wa fedha, David Jackson alisema
kwamba wataalamu walioalikwa wanatarajiwa kutoka na msimamo unahusu uwezeshaji
wa fedha wa ndani.
Alisema wakati dunia inakabiliwa na mabadiliko
makubwa ya wananchi kutoka vijijini kwenda mijini uwezo wa majiji mengi duniani
ikiwamo manispaa ni mdogo kuwezesha kutengeneza miundombinu na pia kuwezesha
ajira.
Alisema kwa sasa kutokana na uwingi
wa watu wanaofurika katika miji, halmashauri na uhaba wa fedha
kutoka katika vyanzo vya mapato kumesababisha kushindwa kuendelezwa mifumo
endelevu ya miundombinu na ajira na kulazimisha wataalamu kuanza kuangalia
namna nyingine ya kupata fedha.
Alisema mpango wa kutafuta vyanzo vingine vya
fedha kwa kuunganisha nguvu nje ya mfumo rasmi umewezekana Tanzania hasa
kutokana na manispaa kama ya Kibaha kuwezeshwa kupata fedha za miradi
mbalimbali na wengine nao watatoa uzoefu wao.
“Zamani ilikuwa rahisi sana kwa manispaa nyingi
kutengeneza mipango ya maendeleo, lakini kwa sasa kutokana na uwingi
wahamaji vyanzo vya kawaida vimezidiwa na kuonekana haja ya kutafuta vyanzo
vingine ili kuwezesha maendeleo na ajira” alisema Jackson.
Alisema mataifa yanahitaji sasa kuangalia mifumo
yao ya kuwezesha maendeleo endelevu kwa kutumia vyanzo vya ndani ambavyo
vinawezekana kupatikana.
Alisema miradi mikubwa ya maendeleo haiwezi
kufanywa na vyanzo vya zamani na kutolea mfano mradi wa maji wa Abudhabi ambao
umewezeshwa kwa kutumia vyanzo vya ndani lakini kwa namna ambayo inasaidia mji
huo kuwa na maji ya uhakika pamoja na kwamba vyanzo vyake havifai.
Alisema ni matumaini yake kwamba baada ya
kusikiliza mada mbalimbali wataalamu hao watakuwa na nafasi ya kutoa tamko la
amna bora ya kushirikisha wadau wa maendeleo wa ndani kutengeneza miradi
mikubwa ya huduma kwa jamii.
Alisema kwamba washiriki katika mkutano huo wa
siku 2 ni pamoja na wadau wa maendeleo kutoka uswis,Sweden na Denmark wapo pia
wataalamu wa masuala ya fedha miradi kutoka Afrika Kusini, Ethiopia, Benin,
Rwanda, mali, Senegal,Uganda, Msumbiji, india, Bangladesh , Marekani na
Tanzania.
Mkutano huo wa mashauriano uliandaliwa na UNCDF
ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa azimio la AddisAbaba kuhusu maendeleo
endelevu na umuhimu wa kuimarisha uwezo wa kifedha wa manispaa mbalimbali.
Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Serikali za Mitaa
nchini Uganda, John Genda Walala, akiongoza mkutano wakati wa asubuhi
Mchumi, John Boex, akitoa mada kwenye ufunguzi
wa mkutano huo wa siku mbili ulioanza Februari 29, 2016
Mshauri wa kujitegemea kutoka nchini India,
Rajivan Krishnaswami, akitoa mada
Mtoa Mada, Suzane Ngane kutoka Cameroun, akitoa mada kwenye mkutano huo
Baadhi yawashiriki wa mkutano
Baadhi yawashiriki wa mkutano
Katibu Mkuu wa Chama Cha Serikali za Mitaa
Tanzania (ALAT), Habraham Shemumoyo, akifuatilia kwa makini mkutano huo
Naibu Mkurugenzi Mtendaji Benki ya TIB, Jaffer
Machano, akitoa mada kwenye mkutano wa siku mbili wa Wataalamu wa fedha na
wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali Duniani, kwenye hoteli ya Hyaatt
Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Februari 29, 2016.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa
Mataifa (UNDCF), David Jackson, (kushoto), akijadiliana jambo na Mshauri wa
kiufundi wa shirika hilo(mpango wa (LFI), hapa nchini, Peter Malika.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269