Breaking News

Your Ad Spot

Feb 2, 2016

VIRUSI VYA ZIKA NI JANGA LA KIMATAIFA; WHO YATANGAZA; NI UGONJWA UNAOENEZWA NA MBU NA KUPELEKEA MTOTO KUZALIWA NA KICHWA KIDOGO

 Baba akiwa amembeba mwanaye aliyezaliwa akiwa ameathirika na Virusi vya ZIKA huko Brazil


NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
UGONJWA wa ZIKA unaoenezwa na virusi vya microcephaly vinavyotoka kwenye Mbu, umetangazwa kuwa ni janga la kimataifa.
Maambukizi ya ZIKA ambayo wataalamu wanahofia kuwa vinasambaa kwa kasi na kuhusishwa na maelfu ya watoto waliozaliwa na udhaifu wa kukua kwa ubongo na hivyo kuathiri ukuaji wa viungo vya mwili.
Tangazo la Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), limeuweka ugonjwa huu kwenye kundi la magonjwa hatari kama EBOLA na itasaidia utafiti ambao utapelekea kupambana na maambukizi..
Tayari Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kuwa Tanzania hakuna tishio la ugonjwa huo lakini akawataka wananchi kuchukua tahadhari na kutoa taarifa mara waonapo motto anazaliwa akiwa na maumbileyasiyo ya kawaida.
Virusi hivi humshambulia mama mjamzito aliyeng’atwa na Mbu mwenye virusi hivyo na hupelekea kuzaa mtotomwenye kicwa kidogo na ubongo mdogo.
Mkuu wa WHO, Margaret Chan, amesema katika tangazo lake kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya vimelea vya ZIKA na microcephaly kuwa ndio vimesababisha janga hilo ingawa bado haijathibitishwa kisayansi.
Ugonjwa wa ZIKA umesambaa sana kwenye nchi za Marekani Kusini hususan Brazil

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages